Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia Zilpa
Mwanzo 29 : 24
24 Labani akampa Lea mjakazi wake Zilpa, awe mjakazi wake.
Mwanzo 30 : 13
13 Lea akasema, Ni heri mimi, maana wanawake wataniita heri. Akamwita jina lake Asheri.
Mwanzo 35 : 26
26 Wana wa Zilpa, kijakazi wa Lea, ni Gadi na Asheri. Hawa ndio wana wa Yakobo aliozaliwa katika Padan-aramu.
Mwanzo 37 : 2
2 Hivi ndivyo vizazi vya Yakobo. Yusufu, aliyekuwa mwenye miaka kumi na saba, alikuwa akichunga kondoo pamoja na ndugu zake; naye alikuwa kijana pamoja na wana wa Bilha, na wana wa Zilpa, wake wa baba yake. Yusufu akamletea baba yao habari zao mbaya.
Mwanzo 46 : 18
18 Hao ndio wana wa Zilpa, ambaye Labani alimpa Lea, binti yake, naye akamzalia Yakobo hao, watu kumi na sita.
Leave a Reply