Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia zawadi
2 Wakorintho 9 : 15
15 Mungu ashukuriwe kwa sababu ya kipawa chake, tusichoweza kukisifu kama ipasavyo.
Warumi 6 : 23
23 Kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti; bali karama ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu.
Yakobo 1 : 17
17 Kila kutoa kuliko kwema, na kila kitolewacho kilicho kamili, hutoka juu, hushuka kwa Baba wa mianga; kwake hakuna kubadilika, wala kivuli cha kugeukageuka.
Mithali 18 : 16
16 Zawadi ya mtu humpatia nafasi; Humleta mbele ya watu wakuu.
Leave a Reply