Biblia inasema nini kuhusu Waziri (2) – Mistari yote ya Biblia kuhusu Waziri (2)

Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia Waziri (2)

Mwanzo 41 : 44
44 Farao akamwambia Yusufu, Mimi ni Farao, na bila amri yako, mtu asiinue mkono wala mguu katika nchi yote ya Misri.

2 Samweli 20 : 26
26 Tena na Ira, Myairi, alikuwa kuhani kwa Daudi.

1 Wafalme 4 : 5
5 ⑫ na Azaria mwana wa Nathani alikuwa afisa mkuu tawala; na Zabudi mwana wa Nathani alikuwa kuhani, rafiki yake mfalme.

1 Mambo ya Nyakati 27 : 33
33 na Ahithofeli alikuwa mshauri wake mfalme; na Hushai, Mwarki, alikuwa rafiki yake mfalme;

2 Mambo ya Nyakati 19 : 11
11 Tena angalieni, Amaria, kuhani mkuu, yuko juu yenu kwa maneno yote ya BWANA; naye Zebadia, mwana wa Ishmaeli, jemadari wa nyumba ya Yuda, kwa mambo yote ya mfalme; Walawi nao watakuwa wasimamizi mbele yenu. Jitieni nguvu, mtende, naye BWANA awe pamoja nao walio wema.

2 Mambo ya Nyakati 28 : 7
7 Naye Zikri, mtu hodari wa Efraimu, akawaua Maaseya mwana wa mfalme, na Azrikamu mkuu wa nyumba, na Elkana, aliyekuwa wa pili wake mfalme.

Esta 3 : 1
1 Baada ya hayo mfalme Ahasuero alimpandisha cheo Hamani mwana wa Hamedatha, Mwagagi,[6] akamwinua, akamwekea kiti chake juu ya wakuu wote waliokuwapo pamoja naye.

Esta 10 : 3
3 Kwa maana Mordekai Myahudi akiwa wa pili wake mfalme Ahasuero, na mkuu wa Wayahudi, amependeza mbele ya jamii ya ndugu zake; ambaye aliwajali watu wake, na kuiangalia hali njema ya wazawa wao wote.

Danieli 2 : 48
48 ③ Basi mfalme akamtukuza Danieli, akampa zawadi kubwa nyingi sana, akamfanya kuwa mkubwa juu ya utawala wote wa Babeli, na kuwa mtawala mkuu juu ya wote wenye hekima wa Babeli.

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *