Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia wavuvi wa watu
Mathayo 4 : 19
19 Akawaambia, Nifuateni, nami nitawafanya kuwa wavuvi wa watu.
Marko 1 : 17
17 Yesu akawaambia, Njooni mnifuate, nami nitawafanya kuwa wavuvi wa watu.
Mathayo 28 : 19
19 Basi, nendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu;
Mathayo 28 : 19 – 20
19 Basi, nendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu;
20 na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi; na tazama, mimi nipo pamoja nanyi siku zote, hata ukamilifu wa dahari.
1 Timotheo 2 : 5
5 Kwa sababu Mungu ni mmoja, na mpatanishi kati ya Mungu na wanadamu ni mmoja, Mwanadamu Kristo Yesu;
Tito 2 : 11
11 Maana neema ya Mungu iwaokoao wanadamu wote imefunuliwa;
Leave a Reply