Biblia inasema nini kuhusu Viwanda – Mistari yote ya Biblia kuhusu Viwanda

Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia Viwanda

Mwanzo 2 : 15
15 BWANA Mungu akamtwaa huyo mtu, akamweka katika bustani ya Edeni, ailime na kuitunza.

Kutoka 23 : 12
12 Siku sita utafanya kazi yako, na siku ya saba utapumzika; ili kwamba ng’ombe wako na punda wako wapate kupumzika, kisha mwana wa mjakazi wako na mgeni wapate kuburudika.

Kumbukumbu la Torati 5 : 13
13 ⑤ Siku sita fanya kazi, utende mambo yako yote;

Kutoka 35 : 2
2 Fanyeni kazi siku sita, lakini siku ya saba itakuwa siku takatifu kwenu; ni Sabato ya kustarehe kabisa kwa BWANA; mtu yeyote atakayefanya kazi yoyote katika siku hiyo atauawa.

Mithali 10 : 5
5 Akusanyaye wakati wa joto ni mwana mwenye hekima; Bali asinziaye wakati wa mavuno ni mwana mwenye kuaibisha.

Mithali 12 : 11
11 Alimaye shamba lake atakuwa na chakula tele; Bali afuataye mambo ya upuzi hana ufahamu.

Mithali 12 : 24
24 ⑥ Mkono wa mwenye bidii utatawala; Bali mvivu atalipishwa kodi.

Mithali 12 : 27
27 Mtu mvivu hapiki mawindo yake; Bali mwenye bidii anazo mali za thamani.

Mithali 13 : 4
4 Nafsi ya mtu mvivu hutamani asipate kitu; Bali nafsi ya mwenye bidii itanenepeshwa.

Mithali 13 : 11
11 ⑭ Mali iliyopatikana kwa haraka itapunguka; Bali yeye achumaye kidogo kidogo atazidishiwa.

Mithali 13 : 23
23 Chakula kingi chapatikana kwa ukulima wa maskini; Bali viko viharibiwavyo kwa sababu ya dhuluma.

Mithali 14 : 4
4 Zizi ni safi ambapo hapana ng’ombe; Bali nguvu za ng’ombe zaleta faida nyingi.

Mithali 14 : 23
23 Katika kila kazi mna faida; Bali maneno ya midomo huleta hasara tu.

Mithali 16 : 26
26 Nafsi yake mfanyakazi hujifanyia kazi; Maana kinywa chake humtia bidii.

Mithali 20 : 13
13 ⑩ Usipende usingizi usije ukawa maskini; Fumbua macho yako nawe utashiba chakula.

Mithali 21 : 5
5 Mawazo ya wenye bidii huuelekea utajiri tu; Bali kila mwenye pupa huuelekea uhitaji.

Mithali 22 : 29
29 Je! Wamwona mtu mwenye bidii katika kazi zake? Huyo atasimama mbele ya wafalme; Hatasimama mbele ya watu wasio na cheo.

Mithali 27 : 27
27 Tena yatakuwapo maziwa ya mbuzi, Ya kukutosha kwa chakula chako, Na chakula cha watu wa nyumbani mwako, Na posho la vijakazi vyako.

Mithali 28 : 19
19 Alimaye shamba lake atakuwa na chakula tele; Bali afuataye mambo ya upuzi atapata umaskini wa kumtosha.

Mithali 30 : 28
28 Mjusi hushika kwa mikono yake; Lakini yumo majumbani mwa wafalme.

Mithali 31 : 27
27 Huangalia sana njia za watu wa nyumbani mwake; Wala hali chakula cha uvivu.

Mhubiri 1 : 3
3 Mtu ana faida gani ya kazi yake yote aifanyayo chini ya jua?

Mhubiri 2 : 11
11 Kisha nikaziangalia kazi zote zilizofanywa kwa mikono yangu, na taabu yote niliyotaabika katika kuzitenda; na tazama, yote ni ubatili na kufukuza upepo, wala faida hakuna chini ya jua.

Mhubiri 2 : 22
22 Kwa maana mtu hupata nini kwa kazi yake yote, na kwa juhudi ya moyo wake alivyojitahidi chini ya jua?

Mhubiri 9 : 10
10 Lolote mkono wako utakalolipata kulifanya, ulifanye kwa nguvu zako; kwa kuwa hakuna kazi, wala shauri, wala maarifa, wala hekima, huko kuzimu uendako wewe.

Mhubiri 11 : 4
4 Mwenye kuuangalia upepo hatapanda; Naye ayatazamaye mawingu hatavuna.

Mhubiri 11 : 6
6 Asubuhi panda mbegu zako, Wala jioni usiulegeze mkono wako. Kwa maana wewe hujui ni zipi zitakazofanikiwa, kama ni hii au hii, au kama zote zitafaa sawasawa.

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *