Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia ushauri
Mithali 13 : 10
10 Kiburi huleta mashindano tu; Bali hekima hukaa nao wanaoshauriana.
Mithali 15 : 22
22 Pasipo ushauri mipango vuhunjika; Bali kwa wingi wa washauri huthibitika.
Mithali 20 : 5
5 Mashauri ya moyoni ni kama kilindi; Lakini mtu mwenye ufahamu atayateka.
Yohana 16 : 13
13 ⑮ Lakini yeye atakapokuja, huyo Roho wa kweli, atawaongoza awatie kwenye kweli yote; kwa maana hatanena kwa shauri lake mwenyewe, lakini yote atakayoyasikia atayanena, na mambo yajayo atawapasha habari yake.
2 Timotheo 3 : 16 – 17
16 Kila andiko, lenye pumzi ya Mungu, lafaa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kwa kuwaadibisha katika haki;
17 ili mtu wa Mungu awe kamili, amekamilishwa apate kutenda kila tendo jema.
Mithali 12 : 18
18 Kuna anenaye bila kufikiri, kama kuchoma kwa upanga; Bali ulimi wa mwenye haki ni afya.
Luka 16 : 31
31 Akamwambia, Wasipowasikia Musa na manabii, hawatashawishika hata mtu akifufuka katika wafu.
Mithali 1 : 1 – 3
1 Mithali za Sulemani, mwana wa Daudi, mfalme wa Israeli.
2 Kujua hekima na adabu; kutambua maneno ya ufahamu;
3 kufundishwa matendo ya busara, katika haki na hukumu na adili.
Leave a Reply