Biblia inasema nini kuhusu ushauri – Mistari yote ya Biblia kuhusu ushauri

Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia ushauri

Mithali 13 : 10
10 Kiburi huleta mashindano tu; Bali hekima hukaa nao wanaoshauriana.

Mithali 15 : 22
22 Pasipo ushauri mipango vuhunjika; Bali kwa wingi wa washauri huthibitika.

Mithali 20 : 5
5 Mashauri ya moyoni ni kama kilindi; Lakini mtu mwenye ufahamu atayateka.

Yohana 16 : 13
13 ⑮ Lakini yeye atakapokuja, huyo Roho wa kweli, atawaongoza awatie kwenye kweli yote; kwa maana hatanena kwa shauri lake mwenyewe, lakini yote atakayoyasikia atayanena, na mambo yajayo atawapasha habari yake.

2 Timotheo 3 : 16 – 17
16 Kila andiko, lenye pumzi ya Mungu, lafaa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kwa kuwaadibisha katika haki;
17 ili mtu wa Mungu awe kamili, amekamilishwa apate kutenda kila tendo jema.

Mithali 12 : 18
18 Kuna anenaye bila kufikiri, kama kuchoma kwa upanga; Bali ulimi wa mwenye haki ni afya.

Luka 16 : 31
31 Akamwambia, Wasipowasikia Musa na manabii, hawatashawishika hata mtu akifufuka katika wafu.

Mithali 1 : 1 – 3
1 Mithali za Sulemani, mwana wa Daudi, mfalme wa Israeli.
2 Kujua hekima na adabu; kutambua maneno ya ufahamu;
3 kufundishwa matendo ya busara, katika haki na hukumu na adili.

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *