Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia Usaliti
Mathayo 26 : 16
16 Tokea wakati huo akawa akitafuta nafasi apate kumsaliti.
Mathayo 26 : 50
50 Yesu akamwambia, Rafiki, fanya ulilolijia. Wakaenda, wakanyosha mikono yao wakamkamata Yesu.
Marko 14 : 11
11 Nao waliposikia walifurahi, wakaahidi kumpa fedha. Akatafuta njia ya kumsaliti wakati wa kufaa.
Luka 22 : 6
6 Akakubali, akatafuta nafasi ya kumsaliti kwao pasipokuwapo mkutano.
Luka 22 : 48
48 Yesu akamwambia, Yuda, wamsaliti Mwana wa Adamu kwa kumbusu?
Yohana 13 : 21
21 Naye alipokwisha kusema hayo, Yesu alifadhaika rohoni, akashuhudia akisema, Amin, amin, nawaambieni, Mmoja wenu atanisaliti.
Mathayo 20 : 18
18 Angalieni, tunapanda kwenda Yerusalemu; na Mwana wa Adamu atatiwa mikononi mwa wakuu wa makuhani na waandishi; nao watamhukumu afe;
Mathayo 24 : 10
10 Ndipo wengi watakapojikwaa, nao watasalitiana, na kuchukiana.
1 Samweli 22 : 10
10 Naye akamwuliza BWANA kwa ajili yake, akampa vyakula, akampa na ule upanga wa Goliathi, Mfilisti.
1 Samweli 21 : 10
10 Basi Daudi akaondoka, akakimbia siku ile, kwa hofu ya Sauli, akamwendea Akishi, mfalme wa Gathi.
Leave a Reply