Biblia inasema nini kuhusu Uchumi – Mistari yote ya Biblia kuhusu Uchumi

Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia Uchumi

Mwanzo 41 : 57
57 Watu wa nchi zote wakaja Misri kwa Yusufu; ili wanunue nafaka; kwa sababu njaa imekuwa nzito katika dunia yote.

Mithali 24 : 27
27 Tengeneza kazi yako huko nje, Jifanyizie kazi yako tayari shambani, Ukiisha, jenga nyumba yako.

Mithali 31 : 31
31 Mpe mapato ya mikono yake, Na matendo yake yamsifu malangoni.

Mhubiri 11 : 6
6 Asubuhi panda mbegu zako, Wala jioni usiulegeze mkono wako. Kwa maana wewe hujui ni zipi zitakazofanikiwa, kama ni hii au hii, au kama zote zitafaa sawasawa.

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *