Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia tulia
Zaburi 46 : 10
10 ⑰ Tulieni, mjue ya kuwa Mimi ni Mungu, Nitakuzwa katika mataifa, nitakuzwa katika nchi.
Kutoka 14 : 14
14 ⑦ BWANA atawapigania ninyi, nanyi mtanyamaza kimya.
Zaburi 37 : 7
7 Utulie mbele za BWANA, Nawe umngojee kwa subira; Usihangaike juu ya afanikiwaye katika njia yake, Wala mtu apangaye maovu.
Marko 4 : 39
39 Akaamka, akaukemea upepo, akaiambia bahari, Nyamaza, utulie. Upepo ukakoma, kukawa shwari kuu.
Zaburi 23 : 1 – 6
1 BWANA ndiye mchungaji wangu, Sitapungukiwa na kitu.
2 Katika malisho ya majani mabichi hunilaza, Kando ya maji ya utulivu huniongoza.
3 Hunihuisha nafsi yangu; na kuniongoza Katika njia za haki kwa ajili ya jina lake.
4 Naam, nijapopita kati ya bonde la kivuli cha mauti, Sitaogopa mabaya; Kwa maana Wewe upo pamoja nami, Gongo lako na fimbo yako vyanifariji.
5 Waandaa meza mbele yangu, Machoni pa watesi wangu. Umenipaka mafuta kichwani pangu, Na kikombe changu kinafurika.
6 Hakika wema na fadhili zitanifuata Siku zote za maisha yangu; Nami nitakaa nyumbani mwa BWANA milele.
Zaburi 62 : 5
5 Nafsi yangu, umngoje Mungu peke yake kwa utulivu. Maana tumaini langu hutoka kwake.
Zaburi 131 : 2
2 ⑬ Hakika nimeituliza nafsi yangu, Na kuinyamazisha. Kama mtoto aliyeachishwa kunyonya Kifuani mwa mama yake; Roho yangu ni kama mtoto, Aliyeachishwa kunyonya.
Ayubu 6 : 24
24 ⑲ Nifunzeni, nami nitanyamaa kimya; Mkanijulishe ni jambo gani nililokosa.
Zaburi 1 : 1 – 6
1 Heri mtu yule asiyekwenda Katika shauri la wasio haki; Wala hakusimama katika njia ya wenye dhambi; Wala hakuketi barazani pa wenye mizaha.
2 Bali sheria ya BWANA ndiyo impendezayo, Na sheria yake huitafakari mchana na usiku.
3 Naye atakuwa kama mti uliopandwa Kandokando ya vijito vya maji, Uzaao matunda yake kwa majira yake, Wala jani lake halinyauki; Na kila alitendalo litafanikiwa.
4 Sivyo walivyo wasio haki; Hao ni kama makapi yapeperushwayo na upepo.
5 Kwa hiyo wasio haki hawatasimama hukumuni, Wala wakosaji katika kusanyiko la wenye haki.
6 Kwa kuwa BWANA anaijua njia ya wenye haki, Bali njia ya wasio haki itapotea.
Zaburi 91 : 1 – 16
1 Aketiye mahali pa siri pake Aliye Juu Atakaa katika uvuli wake Mwenyezi.
2 Atasema, BWANA ndiye kimbilio langu na ngome yangu, Mungu wangu nitakayemtumaini.
3 Maana Yeye atakuokoa kutoka kwa mtego wa mwindaji, Na katika maradhi mabaya.
4 ⑳ Kwa manyoya yake atakufunika, Chini ya mbawa zake utapata kimbilio; Uaminifu wake ni ngao na kigao.
5 Hutaogopa hatari za usiku, Wala mshale urukao mchana,
6 Wala mapigo yajayo usiku, Wala maafa yatokeayo adhuhuri,
7 Hata watu elfu wakianguka ubavuni pako. Naam, watu elfu kumi katika mkono wako wa kulia! Wewe hutakaribiwa na maafa.
8 Ila kwa macho yako utatazama, Na kuyaona malipo ya wasio haki.
9 Kwa kuwa Wewe BWANA ndiwe kimbilio langu; Umemfanya Aliye Juu kuwa makao yako.
10 Mabaya hayatakupata wewe, Wala tauni haitaikaribia hema yako.
11 Kwa kuwa atakuagizia malaika wake Wakulinde katika njia zako zote.
12 Mikononi mwao watakuchukua, Usije ukajikwaa mguu wako katika jiwe.
13 Utawakanyaga simba na nyoka, Mwanasimba na joka utawakanyaga kwa miguu.
14 Kwa kuwa amekaza kunipenda Nitamwokoa; na kumweka palipo juu, Kwa kuwa amenijua Jina langu.
15 Ataniita nami nitamwitikia; Nitakuwa pamoja naye taabuni, Nitamwokoa na kumtukuza;
16 Kwa siku nyingi nitamshibisha, Nami nitamwonesha wokovu wangu.
1 Petro 3 : 4
4 bali kuwe utu wa moyoni usioonekana, katika mapambo yasiyoharibika; yaani, roho ya upole na utulivu, iliyo ya thamani kuu mbele za Mungu.
Habakuki 2 : 1
1 Mimi nitasimama katika zamu yangu, nitajiweka juu ya mnara, nitaangalia ili nione atakaloniambia, na jinsi nitakavyojibu kuhusu kulalamika kwangu.
Zaburi 34 : 1 – 22
1 Nitamhimidi BWANA kila wakati, Sifa zake zi kinywani mwangu daima.
2 ① Katika BWANA nafsi yangu itajisifu, Wanyenyekevu wasikie na kufurahi.
3 Mtukuzeni BWANA pamoja nami, Na tuliadhimishe jina lake pamoja.
4 ② Nilimtafuta BWANA, naye akanijibu, Akaniokoa kutoka kwa hofu zangu zote.
5 Mwelekezeeni macho, mpate kufurahi, Na nyuso zenu hazitaaibishwa kamwe.
6 ③ Maskini huyu aliita, BWANA akasikia, Akamwokoa na taabu zake zote.
7 ④ Malaika wa BWANA huwazungukia, Wamchao na kuwaokoa.
8 ⑤ Onjeni muone ya kuwa BWANA yu mwema; Heri mtu yule anayemtumainia.
9 ⑥ Mcheni BWANA, enyi watakatifu wake, Maana, wamchao hawapungukiwi kitu.
10 Wanasimba hutindikiwa, na kuona njaa; Bali wamtafutao BWANA hawapungukiwi kitu chochote kilicho chema.
11 Njoni, enyi wana, mnisikilize, Nami nitawafundisha kumcha BWANA.
12 ⑦ Ni nani atamaniye uzima na atakaye kuishi, Siku nyingi afurahie mema?
13 ⑧ Uuzuie ulimi wako na mabaya, Na midomo yako na kusema hila.
14 Uache mabaya ukatende mema, Utafute amani ukaifuatie.
15 ⑩ Macho ya BWANA huwaelekea wenye haki, Na masikio yake hukielekea kilio chao.
16 ⑪ Uso wa BWANA ni juu ya watenda mabaya, Aliondoe kumbukumbu lao duniani.
17 Walilia, naye BWANA akasikia, Akawaponya kutoka kwa taabu zao zote.
18 BWANA yu karibu nao waliovunjika moyo, Na huwaokoa waliopondeka roho.
19 Mateso ya mwenye haki ni mengi, Lakini BWANA kutoka kwayo yote.
20 ⑫ Huihifadhi mifupa yake yote, Usivunjike hata mmoja.
21 ⑬ Uovu utamwua asiye haki, Nao wamchukiao mwenye haki watahukumiwa.
22 ⑭ BWANA huzikomboa nafsi za watumishi wake, Wote wamkimbiliao hawatahukumiwa.
Zaburi 46 : 1 – 11
1 Mungu kwetu sisi ni kimbilio na nguvu, Msaada utakaoonekana tele wakati wa mateso.
2 Kwa hiyo hatutaogopa ijapobadilika nchi, Ijapotetemeka milima moyoni mwa bahari.
3 Maji yake yajapovuma na kuumuka, Ijapopepesuka milima kwa kiburi chake.
4 ⑮ Kuna mto, vijito vyake vyaufurahisha mji wa Mungu, Patakatifu pa maskani zake Aliye Juu.
5 ⑯ Mungu yu katikati ya mji hautatetemeshwa; Mungu atausaidia asubuhi na mapema.
6 Mataifa yanaghadhibika na falme kutetemeka; Anatoa sauti yake, nchi inayeyuka.
7 BWANA wa majeshi yu pamoja nasi, Mungu wa Yakobo ni ngome yetu.
8 Njoni muyatazame matendo ya BWANA, Jinsi alivyofanya ukiwa katika nchi.
9 Avikomesha vita hata mwisho wa dunia; Avunja uta, akata mkuki, achoma moto magari.
10 ⑰ Tulieni, mjue ya kuwa Mimi ni Mungu, Nitakuzwa katika mataifa, nitakuzwa katika nchi.
11 BWANA wa majeshi yu pamoja nasi, Mungu wa Yakobo ni kimbilio[8] letu.
1 Wathesalonike 4 : 11
11 ⑰ Tena mjitahidi kutulia, na kutenda shughuli zenu, na kufanya kazi kwa mikono yenu wenyewe, kama tulivyowaagiza;
Isaya 32 : 17
17 ⑦ Na kazi ya haki itakuwa amani; na mazao ya haki yatakuwa ni utulivu na matumaini daima.
Maombolezo 3 : 24 – 26
24 BWANA ndiye fungu langu, husema nafsi yangu, Kwa hiyo nitamtumaini yeye.
25 BWANA ni mwema kwa hao wamngojeao, Kwa hiyo nafsi imtafutayo.
26 Ni vema mtu autarajie wokovu wa BWANA Na kumngojea kwa utulivu.
1 Wafalme 19 : 11 – 13
11 ① Akasema, Toka, usimame mlimani mbele za BWANA. Na tazama, BWANA akapita; upepo mwingi wa nguvu ukaipasua milima, ukaivunjavunja miamba mbele za BWANA; lakini BWANA hakuwamo katika upepo ule; na baada ya upepo, tetemeko la nchi; lakini BWANA hakuwamo katika lile tetemeko la nchi;
12 ② na baada ya tetemeko la nchi kukawa na moto; lakini BWANA hakuwamo katika moto ule; na baada ya moto sauti ndogo, ya utulivu.
13 ③ Ikawa, Eliya alipoisikia, alijifunika uso wake katika mavazi yake, akatoka, akasimama mlangoni mwa pango. Na tazama, sauti ikamjia, kusema, Unafanya nini hapa, Eliya?
Leave a Reply