Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia theluji
Isaya 1 : 18
18 Haya, njoni, tusemezane, asema BWANA. Dhambi zenu zijapokuwa nyekundu sana, zitakuwa nyeupe kama theluji; zijapokuwa nyekundu kama damu, zitakuwa kama sufu.
Mathayo 28 : 3
3 Na sura yake ilikuwa kama umeme, na mavazi yake meupe kama theluji.
Zaburi 51 : 7
7 Unisafishe kwa hisopo nami nitakuwa safi, Unioshe, nami nitakuwa mweupe kuliko theluji.
Ufunuo 1 : 14
14 Kichwa chake na nywele zake zilikuwa nyeupe kama sufu nyeupe, kama theluji; na macho yake kama muali wa moto;
Zaburi 68 : 14
14 Mwenyezi Mungu alipotawanya wafalme huko, Kulinyesha theluji katika Salmoni.
Hesabu 12 : 10
10 ⑥ Kisha hilo wingu likaondoka kutoka pale juu ya hema; na tazama, Miriamu akawa mwenye ukoma, mweupe kama theluji; Haruni akamwangalia Miriamu, na na kumwona akiwa mwenye ukoma.
Leave a Reply