Biblia inasema nini kuhusu tai – Mistari yote ya Biblia kuhusu tai

Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia tai

Isaya 40 : 29 – 31
29 Huwapa nguvu wazimiao, humwongezea nguvu yeye asiyekuwa na uwezo.
30 Hata vijana watazimia na kuchoka, na vijana wanaume wataanguka;
31 bali wao wamngojeao BWANA watapata nguvu mpya; watapanda juu kwa mbawa kama tai; watakimbia, wala hawatachoka; watakwenda kwa miguu, wala hawatazimia.

Mithali 23 : 5
5 Je! Utavikazia macho vile ambavyo si kitu? Maana bila shaka mali hujifanyia mabawa, Kama tai arukaye mbinguni.

Kumbukumbu la Torati 32 : 11
11 Mfano wa tai ataharikishaye kioto chake; Na kupapatika juu ya makinda yake, Alikunjua mbawa zake, akawatwaa, Akawachukua juu ya mbawa zake;

Mambo ya Walawi 11 : 13
13 ⑥ Kisha katika ndege hawa watakuwa ni machukizo kwenu; hawataliwa, ndio machukizo; tai, na furukombe, na kipungu;

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *