Biblia inasema nini kuhusu Taa – Mistari yote ya Biblia kuhusu Taa

Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia Taa

Mwanzo 15 : 17
17 Ikawa, jua lilipokuchwa likawa giza, tazama, tanuri ya moshi na mwenge unaowaka ulipita kati ya vile vipande vya nyama.

Kutoka 25 : 40
40 Nawe angalia ya kwamba uvifanye kama mfano wake, uliooneshwa mlimani.

Kutoka 37 : 22
22 Hayo matovu yake na matawi yake yalikuwa ya kitu kimoja nacho; kinara hicho kizima chote pia ni kazi moja ya kufua ya dhahabu safi.

Kutoka 27 : 21
21 ⑳ Ndani ya ile hema ya kukutania, nje ya hilo pazia, lililo mbele ya huo ushuhuda, Haruni na wanawe wataitengeza tangu jioni hadi asubuhi mbele ya BWANA; itakuwa ni amri ya milele katika vizazi vyao vyote kwa ajili ya wana wa Israeli.

Mambo ya Walawi 24 : 4
4 Atazitengeneza hizo taa katika kile kinara kilicho safi mbele za BWANA daima.

Ayubu 18 : 6
6 Mwanga hemani mwake utakuwa giza, Nayo taa iliyo juu yake itazimwa.

Zaburi 119 : 105
105 Neno lako ni taa ya miguu yangu, Na mwanga wa njia yangu.

Mithali 13 : 9
9 Nuru ya mwenye haki yang’aa sana; Bali taa ya mtu mbaya itazimika.

Mithali 20 : 20
20 ⑪ Amlaaniye babaye au mamaye, Taa yake itazimika katika giza kuu.

Isaya 62 : 1
1 Kwa ajili ya Sayuni sitanyamaza, na kwa ajili ya Yerusalemu sitatulia, hata haki yake itakapotokea kama mwangaza, na wokovu wake kama taa iwakayo.

Yeremia 25 : 10
10 Tena, nitawaondolea sauti ya kicheko, na sauti ya furaha, sauti ya bwana arusi, na sauti ya bibi arusi, sauti ya mawe ya kusagia, na nuru ya mishumaa.

Sefania 1 : 12
12 Kisha itakuwa wakati ule, nitauchunguza Yerusalemu kwa taa; nami nitawaadhibu watu walioganda juu ya masira yao; wasemao katika mioyo yao, BWANA hatatenda mema, wala hatatenda mabaya.

Mathayo 6 : 22
22 ① Taa ya mwili ni jicho; basi jicho lako likiwa kamili, mwili wako wote utakuwa na nuru.

2 Petro 1 : 19
19 Nasi tuna lile neno la unabii lililo imara zaidi, ambalo, mkiliangalia, kama taa iangazayo mahali penye giza, mwafanya vyema, mpaka kutakapopambazuka, na nyota ya asubuhi kuzuka mioyoni mwenu.

Ufunuo 21 : 23
23 ⑯ Na mji ule hauhitaji jua wala mwezi kuuangaza, kwa maana utukufu wa Mungu huutia nuru, na taa yake ni Mwana-kondoo.

Ufunuo 4 : 5
5 Na katika kile kiti cha enzi kunatoka umeme na sauti na ngurumo. Na taa saba za moto zikiwaka mbele ya kile kiti cha enzi, ndizo Roho saba za Mungu.

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *