Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia mwanariadha
2 Timotheo 4 : 7
7 Nimevipiga vita vilivyo vizuri, mwendo nimeumaliza, Imani nimeilinda;
2 Timotheo 2 : 5
5 Hata mwanariadha hapewi taji, asiposhindana kwa kufuata sheria.
Mithali 27 : 17
17 Chuma hunoa chuma; Ndivyo mtu aunoavyo uso wa rafiki yake.
Isaya 40 : 29 – 31
29 Huwapa nguvu wazimiao, humwongezea nguvu yeye asiyekuwa na uwezo.
30 Hata vijana watazimia na kuchoka, na vijana wanaume wataanguka;
31 bali wao wamngojeao BWANA watapata nguvu mpya; watapanda juu kwa mbawa kama tai; watakimbia, wala hawatachoka; watakwenda kwa miguu, wala hawatazimia.
Zaburi 60 : 12
12 ⑲ Kwa msaada wa Mungu tutatenda makuu, Maana Yeye atawakanyaga watesi wetu.
Zaburi 62 : 2
2 Yeye tu ndiye mwamba wangu na wokovu wangu, Ngome yangu, sitatikisika.
Leave a Reply