Biblia inasema nini kuhusu Mtendaji – Mistari yote ya Biblia kuhusu Mtendaji

Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia Mtendaji

Mathayo 7 : 21
21 Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni.

Mathayo 12 : 50
50 Kwa maana yeyote atakayeyafanya mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni, huyu ndiye kaka yangu, na dada yangu na mama yangu.

Luka 11 : 28
28 ⑳ Lakini yeye alisema, Afadhali, heri walisikiao neno la Mungu na kulishika.

Warumi 2 : 15
15 ⑥ Hao waionesha kazi ya torati iliyoandikwa mioyoni mwao, dhamiri yao ikiwashuhudia, na mawazo yao, yenyewe kwa yenyewe, yakiwashitaki au kuwatetea;

2 Wakorintho 8 : 11
11 Lakini sasa timizeni kule kutenda nako, ili kama vile mlivyokuwa tayari kutamani kutenda, vivyo hivyo mkawe tayari na kutimiza, kwa kadiri ya mlivyo navyo.

Yakobo 1 : 27
27 Dini iliyo safi, isiyo na dosari mbele za Mungu Baba ni hii, Kwenda kuwatazama yatima na wajane katika dhiki yao, na kujilinda na dunia pasipo mawaa.

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *