Biblia inasema nini kuhusu Milele – Mistari yote ya Biblia kuhusu Milele

Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia Milele

Isaya 57 : 15
15 Maana yeye aliye juu, aliyetukuka, akaaye milele; ambaye jina lake ni Mtakatifu; asema hivi; Nakaa mimi mahali palipoinuka, palipo patakatifu; tena pamoja na yeye aliye na roho iliyotubu na kunyenyekea, ili kuzifufua roho za wanyenyekevu, na kuifufua mioyo yao waliotubu.

Mika 5 : 2
2 ④ Bali wewe, Bethlehemu Efrata, uliye mdogo kuwa miongoni mwa elfu za Yuda; kutoka kwako wewe atanitokea mmoja atakayekuwa mtawala katika Israeli; ambaye asili yake imekuwa tangu zamani za kale, tangu milele.

Zaburi 30 : 12
12 Ili nafsi yangu ikusifu, Wala isinyamaze. Ee BWANA, Mungu wangu, Nitakushukuru milele.

Zaburi 41 : 13
13 Na atukuzwe BWANA, Mungu wa Israeli, Tangu milele hata milele. Amina na Amina.

Zaburi 72 : 17
17 Jina lake na lidumu milele, Pindi ling’aapo jua, umaarufu wake uwepo; Mataifa yote na wabarikiwe katika yeye, Na kumwita heri.

Zaburi 90 : 2
2 ⑩ Kabla haijazaliwa milima, wala hujaiumba dunia, Na tangu milele hata milele ndiwe Mungu.

Zaburi 110 : 4
4 ⑦ BWANA ameapa, Wala hataghairi, Ndiwe kuhani hata milele, Kwa mfano wa Melkizedeki.

Zaburi 119 : 142
142 ⑬ Haki yako ni haki ya milele, Na sheria yako ni kweli.

Mathayo 6 : 13
13 Na usitutie majaribuni, lakini utuokoe na yule mwovu. [Kwa kuwa ufalme ni wako, na nguvu, na utukufu, hata milele. Amina.]

Mathayo 18 : 8
8 Basi mkono wako au mguu wako ukikukosesha, ukate ukautupe mbali nawe; ni afadhali kuingia katika uzima ukiwa umepungukiwa na mkono au mguu, kuliko kuwa na mikono miwili au miguu miwili, na kutupwa katika moto wa milele.

2 Wakorintho 9 : 9
9 kama ilivyoandikwa, Ametapanya, amewapa maskini, Haki yake yakaa milele.

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *