Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia Mgeni
Mithali 23 : 3
3 Usivitamani vyakula vyake vya anasa; Kwa maana ni vyakula vya hila.
Mithali 23 : 8
8 Tonge lile ulilokula utalitapika, Na maneno yako matamu yatakupotea.
Mithali 25 : 7
7 Kwa maana ni heri kuambiwa, Njoo huku mbele; Kuliko kuwekwa nyuma machoni pa mkuu. Yale uliyoyaona kwa macho,
Mithali 25 : 17
17 Mguu wako usiingie katika nyumba ya jirani yako ila kwa kiasi; Asije akakukinai na kukuchukia.
Luka 10 : 7
7 Basi, kaeni katika nyumba iyo hiyo, mkila na kunywa vya kwao; maana, mfanya kazi amestahili kupewa ujira wake. Msihamahame kutoka nyumba hii kwenda nyumba hii.
Luka 14 : 11
11 Kwa maana kila ajikwezaye atadhiliwa, naye ajidhiliye atakwezwa.
Leave a Reply