Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia lewiathani
Isaya 27 : 1
1 Katika siku hiyo BWANA, kwa upanga wake ulio mkali, ulio mkubwa, ulio na nguvu, atamwadhibu Lewiathani, nyoka yule mwepesi, na Lewiathani, nyoka yule mwenye kuzongazonga; naye atamwua yule joka aliye baharini.
Ayubu 41 : 1 – 34
1 Je! Waweza wewe kumvua mamba kwa ndoana? Au, kuufunga ulimi wake kwa kamba?
2 Je! Waweza kutia kamba puani mwake? Au kutoboa taya yake kwa kulabu?
3 Je! Atakusihi sana? Au, atakuambia maneno ya upole?
4 Je! Atafanya agano pamoja nawe, Umtwae kuwa mtumishi wako milele?
5 Je! Utamchezea kama ndege? Au, kumfunga kwa ajili ya wasichana wako?
6 Je! Vikosi vya wavuvi watamfanyia biashara? Watamgawanya kati ya wafanyao biashara?
7 Je! Waweza kuijaza ngozi yake kwa vyuma vyenye ncha, Au kichwa chake kwa vyusa?
8 Mwekee mkono wako; Vikumbuke vile vita, wala usifanye tena.
9 Tazama, kumtamani ni bure; Je! Hatambwaga chini huyo atakayemtazama?
10 Hapana aliye mkali hata akathubutu kumwamsha; Bali ni nani awezaye kusimama mbele yangu mimi?
11 Ni nani aliyetangulia kunipa hata nimlipe? Kila kilicho chini ya mbingu nzima ni changu.
12 Sitanyamaa kusema habari za via vyake, Wala nguvu zake kuu, wala umbo lake zuri.
13 Ni nani awezaye kumbambua magamba yake? Ni nani atakayepenya dirii yake maradufu?
14 Ni nani awezaye kuifungua milango ya uso wake? Meno yake yatisha kandokando yake.
15 Magamba yake yenye nguvu ndiyo fahari yake, Yamefungamana pamoja kama yaliyofungwa kwa mhuri.
16 Jinsi yalivyoshikamana Hata upepo hauwezi kupita kati.
17 Yamefungamana pamoja; Yameshikamana, hata hayawezi kutengwa.
18 Kwa kuchemua kwake mwanga humemetuka, Na macho yake yanafanana na koze za alfajiri.
19 Mienge iwakayo hutoka kinywani mwake, Na cheche za moto huruka nje.
20 Moshi hutoka katika mianzi ya pua yake, Kama nyungu ikitokota, na manyasi yawakayo.
21 Pumzi zake huwasha makaa, Na miali ya moto hutoka kinywani mwake.
22 Katika shingo yake hukaa nguvu, Na utisho hucheza mbele yake.
23 Minofu ya nyama yake hushikamana; Yanakazana juu yake; hayawezi kuondolewa.
24 Moyo wake una uimara kama jiwe; Naam, uimara kama jiwe la chini la kusagia.
25 Anapojiinua, mashujaa huogopa; Kwa sababu ya woga wao huvunjwa moyo.
26 Mtu akimpiga kwa upanga, haumwingii; Wala fumo, wala mshale, wala mkuki wenye ncha.
27 Yeye huona chuma kuwa kama nyasi, Na shaba kama mti uliooza.
28 Mshale hauwezi kumkimbiza; Na mawe ya teo kwake hugeuka kuwa kama makapi.
29 Marungu huhesabiwa kama mabua; Naye hucheka mshindo wa mkuki ukitupwa.
30 Pande zake za chini ni kama vigae vikali; Hutandika malazi kama kuweka chombo cha kupuria nafaka juu ya matope.
31 Yeye hufanya kilindi kichemke kama chungu; Hufanya bahari kuwa kama chungu cha mafuta.
32 Hufanya mapito yake kung’aa nyuma yake Hata mtu angedhani kilindi kina mvi.
33 Juu ya nchi hapana aliyefanana naye, kiumbe asiye na woga.
34 Yeye hutazama kila kitu kilicho juu; Ni mfalme juu ya wote wenye kiburi.
Zaburi 104 : 26
26 Ndimo zipitamo merikebu, Ndimo alimo Lewiathani uliyemwumba acheze humo.
Zaburi 74 : 14
14 Wewe ulivivunja vichwa vya Lewiathani, Awe chakula cha watu wa jangwani.
Ayubu 41 : 1
1 Je! Waweza wewe kumvua mamba kwa ndoana? Au, kuufunga ulimi wake kwa kamba?
Ayubu 3 : 8
8 Na waulaani hao waulaanio mchana, Hao walio tayari kumwamsha huyo Lewiathani.
Ufunuo 20 : 2
2 Akalishika lile joka, yule nyoka wa zamani, ambaye ni Ibilisi na Shetani, akamfunga miaka elfu;
Zaburi 18 : 8
8 Kukapanda moshi kutoka puani mwake, Moto wa kuteketeza ukatoka kinywani mwake, Makaa ya moto yakamtoka.
Zaburi 74 : 13 – 14
13 Wewe umeipasua bahari kwa nguvu zako, Umevivunja vichwa vya nyangumi juu ya maji.
14 Wewe ulivivunja vichwa vya Lewiathani, Awe chakula cha watu wa jangwani.
Ayubu 41 : 18
18 Kwa kuchemua kwake mwanga humemetuka, Na macho yake yanafanana na koze za alfajiri.
Ayubu 40 : 15 – 24
15 Mwangalie huyo kiboko, niliyemwumba pamoja nawe; Yeye hula nyasi kama ng’ombe,
16 Tazama basi, nguvu zake zimo katika viuno vyake, Na uwezo wake u katika mishipa ya tumbo lake.
17 Yeye hutikisa mkia wake mfano wa mwerezi; Mishipa ya mapaja yake yanaungamana pamoja.
18 Mifupa yake ni kama mirija ya shaba; Mbavu zake ni kama vipande vya chuma.
19 Yeye ni wa kwanza kwa hayo matendo makuu ya Mungu; Ni Muumba wake tu awezaye kumkabili kwa upanga wake.
20 Hakika milima humtolea chakula; Hapo wachezapo wanyama pori wote.
21 Hulala chini ya miti yenye vivuli, Mafichoni penye mianzi, na matopeni.
22 Hiyo miti yenye vivuli humfunika kwa vivuli vyao; Mierebi ya vijito humzunguka.
23 Tazama, mto ukifurika, yeye hatetemeki; Hujiona yu salama, ijapokuwa Yordani hufurika hata kinywani pake.
24 Je! Mtu yeyote atamnasa akiwa yu macho, Au, kumtoboa pua yake kwa mtego?
Ufunuo 13 : 1
1 ① Kisha nikaona mnyama akitoka katika bahari, alikuwa na pembe kumi, na vichwa saba, na juu ya pembe zake ana vilemba kumi, na juu ya vichwa vyake majina ya kukufuru.
Ayubu 41 : 32
32 Hufanya mapito yake kung’aa nyuma yake Hata mtu angedhani kilindi kina mvi.
Ayubu 41 : 31
31 Yeye hufanya kilindi kichemke kama chungu; Hufanya bahari kuwa kama chungu cha mafuta.
Ayubu 41 : 30
30 Pande zake za chini ni kama vigae vikali; Hutandika malazi kama kuweka chombo cha kupuria nafaka juu ya matope.
Ayubu 40 : 21 – 23
21 Hulala chini ya miti yenye vivuli, Mafichoni penye mianzi, na matopeni.
22 Hiyo miti yenye vivuli humfunika kwa vivuli vyao; Mierebi ya vijito humzunguka.
23 Tazama, mto ukifurika, yeye hatetemeki; Hujiona yu salama, ijapokuwa Yordani hufurika hata kinywani pake.
Zaburi 74 : 13
13 Wewe umeipasua bahari kwa nguvu zako, Umevivunja vichwa vya nyangumi juu ya maji.
Mwanzo 1 : 21
21 Mungu akaumba nyangumi wakubwa, na kila kiumbe chenye uhai kiendacho, ambavyo maji yalijawa navyo kwa wingi kwa jinsi zao, na kila ndege arukaye, kwa jinsi yake; Mungu akaona ya kuwa ni vyema.
Leave a Reply