Biblia inasema nini kuhusu kuzidiwa – Mistari yote ya Biblia kuhusu kuzidiwa

Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia kuzidiwa

Zaburi 34 : 17 – 20
17 Walilia, naye BWANA akasikia, Akawaponya kutoka kwa taabu zao zote.
18 BWANA yu karibu nao waliovunjika moyo, Na huwaokoa waliopondeka roho.
19 Mateso ya mwenye haki ni mengi, Lakini BWANA kutoka kwayo yote.
20 ⑫ Huihifadhi mifupa yake yote, Usivunjike hata mmoja.

Wafilipi 4 : 19
19 Na Mungu wangu atawajazeni kila mnachokihitaji kwa kadiri ya utajiri wake, katika utukufu, ndani ya Kristo Yesu.

2 Wakorintho 12 : 9
9 Naye akaniambia, Neema yangu yakutosha; maana uweza wangu hutimilika katika udhaifu. Basi nitajisifia udhaifu wangu kwa furaha nyingi, ili uweza wa Kristo ukae juu yangu.

Mathayo 19 : 26
26 Yesu akawakazia macho, akawaambia, Kwa wanadamu hilo haliwezekani; bali kwa Mungu yote yawezekana.

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *