Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia kuwavunjia heshima wazazi
Waefeso 6 : 1 – 3
1 Enyi watoto, watiini wazazi wenu katika Bwana, maana hii ndiyo haki.
2 ① Waheshimu baba yako na mama yako; hii ndiyo amri ya kwanza yenye ahadi,
3 Upate heri na kuishi siku nyingi katika dunia.
Wakolosai 3 : 20
20 Ninyi watoto, watiini wazazi wenu katika mambo yote; maana jambo hili lapendeza katika Bwana.
Yeremia 31 : 34
34 ⑯ Wala hawatamfundisha kila mtu jirani yake, na kila mtu ndugu yake, wakisema, Mjue BWANA; kwa maana watanijua wote, tangu mtu aliye mdogo miongoni mwao hadi aliye mkubwa miongoni mwao, asema BWANA; maana nitausamehe uovu wao, wala dhambi yao sitaikumbuka tena.
Waefeso 6 : 1
1 Enyi watoto, watiini wazazi wenu katika Bwana, maana hii ndiyo haki.
Kumbukumbu la Torati 27 : 16
16 ⑧ Na alaaniwe amdharauye baba yake au mama yake. Na watu wote waseme, Amina.
Kutoka 20 : 12
12 Waheshimu baba yako na mama yako; siku zako zipate kuwa nyingi katika nchi upewayo na BWANA, Mungu wako.
Yohana 14 : 15
15 ⑬ Mkinipenda, mtazishika amri zangu.
Wagalatia 5 : 14
14 ⑩ Maana torati yote imetimilika katika neno moja, nalo ni hili, Umpende jirani yako kama nafsi yako.
Leave a Reply