Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia kuwa mfano
1 Timotheo 4 : 12
12 ⑲ Mtu awaye yote asiudharau ujana wako, bali uwe kielelezo kwao waaminio, katika usemi na mwenendo, na katika upendo na imani na usafi.
Tito 2 : 6 – 7
6 Vivyo hivyo na vijana waume uwaonye kuwa na kiasi;
7 katika mambo yote ukijionesha wewe mwenyewe kuwa kielelezo cha matendo mema, na katika mafundisho yako ukionesha usahihi na ustahivu,
1 Petro 2 : 16
16 ⑭ kama walio huru, ila wasioutumia uhuru huo kwa kusitiri ubaya, bali kama watumwa wa Mungu.
Mithali 22 : 6
6 Mlee mtoto katika njia impasayo, Naye hataiacha, hata atakapokuwa mzee.
Mithali 24 : 1 – 2
1 Usiwawaonee wivu watu waovu, Wala usitamani kuwa pamoja nao;
2 Kwa maana moyo wao hufikiri dhuluma, Na midomo yao huongea madhara.
1 Petro 2 : 12
12 ⑪ Muwe na mwenendo mzuri kati ya Mataifa, ili, iwapo huwasingizia kuwa watenda mabaya, wayatazamapo matendo yenu mazuri, wamtukuze Mungu siku ya kujiliwa.
Mathayo 5 : 13
13 ③ Ninyi ni chumvi ya dunia; lakini chumvi ikipoteza ladha yake, ladha hiyo itarudishwa vipi? Haifai tena kabisa, ila kutupwa nje na kukanyagwa na watu.
Wafilipi 3 : 17
17 Ndugu zangu, mnifuate mimi, mkawatazame wao waendao kwa kuufuata mfano tuliowapa ninyi.
Yohana 13 : 15
15 Kwa kuwa nimewapa kielelezo; ili kama mimi nilivyowatendea, nanyi mtende vivyo.
Leave a Reply