Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia Kutokujali
Mambo ya Walawi 23 : 29
29 Kwa kuwa mtu yeyote asiyejinyima siku iyo hiyo, atatengwa na watu wake.
Mambo ya Walawi 26 : 24
24 nami nitawapiga, mara saba kwa ajili ya dhambi zenu.
Kumbukumbu la Torati 29 : 21
21 BWANA atamtenga kwa uovu, kutoka kabila zote za Israeli, kwa laana zote za agano lililoandikwa katika kitabu hiki cha torati.
1 Samweli 15 : 23
23 ⑳ Kwani kuasi ni kama dhambi ya uchawi, Na ukaidi ni kama uovu na kuabudu vinyago; Kwa kuwa umelikataa neno la BWANA, Yeye naye amekukataa wewe usiwe mfalme.
Ayubu 9 : 2
2 Kweli najua kuwa ndivyo hivyo; Lakini mtu huwaje mwenye haki mbele za Mungu?
Ayubu 9 : 4
4 Yeye ni mwenye hekima moyoni, na mwenye uwezo katika nguvu; Ni nani aliyejifanya kuwa mgumu juu yake, naye akafanikiwa?
Ayubu 24 : 13
13 Hawa ni katika hao waliouasi mwanga; Hawazijui njia zake, Wala hawakai katika mapito yake.
Ayubu 33 : 14
14 Kwa kuwa Mungu hunena mara moja, Naam, hata mara ya pili, ijapokuwa mtu hatambui.
Zaburi 7 : 13
13 Naye amemtengenezea silaha za kuua, Akifanya mishale yake kuwa mipini ya moto.
Zaburi 10 : 3
3 Maana mdhalimu hujisifia tamaa ya nafsi yake, Na mwenye choyo humkana BWANA na kumdharau.
Zaburi 32 : 9
9 Msiwe kama farasi wala nyumbu, Wasiokuwa na akili. Kwa matandiko ya lijamu na hatamu Sharti kuwazuia hao, au hawatakukaribia.
Zaburi 50 : 17
17 Maana wewe umechukia maonyo, Na kuyatupa maneno yangu nyuma yako.
Zaburi 50 : 21
21 Ndivyo ulivyofanya, nami nikanyamaza; Ukadhani ya kuwa Mimi ni kama wewe. Lakini nitakukemea; Nitakuhukumu kwa hayo yote.
Zaburi 52 : 1
1 ⑧ Kwa nini kujisifia uovu, Ewe jabari? Wema wa Mungu upo sikuzote.
Zaburi 52 : 7
7 ⑭ Kumbe! Huyu ndiye mtu yule, Asiyemfanya Mungu kuwa kimbilio lake. Aliutumainia wingi wa mali zake, Na kufanya mali kimbilio lake.
Zaburi 58 : 5
5 Asiyeisikiliza sauti ya waganga, Ijapo wanafanya uganga kwa ustadi.
Zaburi 68 : 21
21 Naam, Mungu atakipasua kichwa cha adui zake, Utosi wenye nywele wa mtu afululizaye kukosa.
Zaburi 78 : 8
8 Naam, wasiwe kama baba zao, Kizazi cha ukaidi na uasi. Kizazi kisichojitengeneza moyo, Wala roho yake haikuwa amini kwa Mungu.
Zaburi 81 : 12
12 ① Nikawaacha wakaenda kwa ukaidi wa mioyo yao, Waenende katika mashauri yao.
Zaburi 82 : 5
5 ⑤ Hawajui wala hawafahamu, hutembea gizani; Misingi yote ya nchi imetikisika.
Zaburi 95 : 8
8 ⑤ Msifanye mioyo yenu kuwa migumu; Kama ilivyokuwa huko Meriba Kama siku ile katika Masa jangwani.
Waraka kwa Waebrania 3 : 8
8 ④ Msifanye mioyo yenu kuwa migumu, Kama wakati wa kuasi, Siku ya kujaribiwa katika jangwa,
Zaburi 106 : 25
25 Bali wakanung’unika hemani mwao, Wala hawakuisikiliza sauti ya BWANA.
Zaburi 107 : 12
12 ⑭ Hata akawadhili moyo kwa taabu, Wakajikwaa, wala pasiwe na wa kuwasaidia.
Mithali 1 : 31
31 Kwa hiyo watakula matunda ya njia yao, Watashiba mashauri yao wenyewe.
Mithali 11 : 3
3 Ukamilifu wao wenye haki utawaongoza Bali ukaidi wao wenye fitina utawaangamiza.
Mithali 15 : 10
10 Adhabu kali ina yeye aiachaye njia; Naye achukiaye kukemewa atakufa.
Leave a Reply