Biblia inasema nini kuhusu Kunyang’anywa – Mistari yote ya Biblia kuhusu Kunyang’anywa

Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia Kunyang’anywa

2 Samweli 16 : 4
4 Ndipo mfalme akamwambia Siba, Tazama, yote yaliyokuwa ni mali ya Mefiboshethi ni yako. Siba akasema, Mimi ninasujudu; na nione kibali machoni pako, Ee bwana wangu, mfalme.

1 Wafalme 21 : 16
16 Ikawa Ahabu aliposikia ya kwamba Nabothi amekufa, akaondoka, aliteremkie shamba la mizabibu la Nabothi Myezreeli, ili alitamalaki.

Esta 8 : 1
1 Siku ile mfalme Ahasuero alimpa malkia Esta nyumba yake Hamani, yule adui ya Wayahudi. Mordekai naye akaja mbele ya mfalme; kwa maana Esta alikuwa amedhihirisha alivyomhusu.

Ezra 10 : 8
8 ⑪ na ya kwamba mtu yeyote asiyekuja katika muda wa siku tatu, kwa shauri lile la wakuu na wazee, basi aondolewe mali zake zote, akatengwe yeye mwenyewe na mkutano wa uhamisho.

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *