Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia kulaani wazazi wako
Mambo ya Walawi 20 : 9
9 Kwa maana kila mtu amlaaniye baba yake au mama yake hakika atauawa, amemlaani baba yake na mama yake; damu yake itakuwa juu yake.
Kutoka 21 : 15
15 Ampigaye baba yake au mama yake, sharti atauawa.
Luka 14 : 26
26 ⑥ Kama mtu akija kwangu naye hamchukii baba yake, na mama yake, na mke wake, na wanawe, na ndugu zake wa kiume na wa kike; naam, na hata nafsi yake mwenyewe, hawezi kuwa mwanafunzi wangu. ⑦
Mithali 20 : 20
20 ⑪ Amlaaniye babaye au mamaye, Taa yake itazimika katika giza kuu.
Mathayo 15 : 4
4 Kwa kuwa Mungu alisema, Mheshimu baba yako na mama yako, na Amtukanaye baba yake au mama yake kufa na afe.
Leave a Reply