Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia Kulaani
Kutoka 21 : 17
17 Yeye amwapizaye baba yake au mama yake, sharti atauawa.
Mathayo 15 : 4
4 Kwa kuwa Mungu alisema, Mheshimu baba yako na mama yako, na Amtukanaye baba yake au mama yake kufa na afe.
Marko 7 : 10
10 Maana Musa alisema, Waheshimu baba yako na mama yako, na, Amtukanaye babaye au mamaye kufa na afe.
2 Samweli 16 : 8
8 BWANA amerudisha juu yako damu yote ya nyumba ya Sauli ambaye umetawala badala yake; naye BWANA ametia ufalme katika mkono wa Absalomu mwanao; kisha, angalia, wewe umetwaliwa katika uovu wako mwenyewe, kwa sababu umekuwa mtu wa damu.
Mathayo 5 : 44
44 lakini mimi nawaambia, Wapendeni adui zenu, waombeeni wanaowaudhi,
Luka 6 : 28
28 wabarikieni wale ambao wawalaani ninyi, waombeeni wale ambao wawaonea ninyi.
Leave a Reply