Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia Kiu
Zaburi 42 : 4
4 Nayakumbuka mambo haya kwa uchungu moyoni mwangu, Jinsi nilivyokuwa nikienda na mkutano, Na kuwaongoza hadi katika nyumba ya Mungu, Kwa sauti ya furaha na kusifu, mkutano wa sikukuu.
Zaburi 63 : 1
1 Ee MUNGU, Mungu wangu, nitakutafuta mapema, Nafsi yangu inakuonea kiu, Mwili wangu wakuonea shauku, Katika nchi kame na uchovu, isiyo na maji.
Zaburi 143 : 6
6 Nakunyoshea mikono yangu; Nafsi yangu inakuonea kiu kama nchi kame.
Isaya 55 : 1
1 ⑮ Haya, kila aonaye kiu, njoni majini, Naye asiye na fedha; njoni, nunueni mle; Naam, njoni, nunueni divai na maziwa, Bila fedha na bila gharama.
Amosi 8 : 13
13 Siku hiyo wanawali wazuri na wavulana watazimia kwa kiu.
Mathayo 5 : 6
6 Heri wenye njaa na kiu ya haki; Maana hao watashibishwa.
Yohana 4 : 15
15 Yule mwanamke akamwambia, Bwana, unipe maji hayo, nisione kiu, wala nisije hapa kuteka.
Yohana 7 : 37
37 Katika siku ya mwisho, siku ile kubwa ya sikukuu, Yesu akasimama, akapaza sauti yake akisema, Mtu akiona kiu, na aje kwangu anywe.
Ufunuo 21 : 6
6 ④ Akaniambia, Imekwisha kuwa. Mimi ni Alfa na Omega, Mwanzo na Mwisho. Mimi nitampa yeye aliye na kiu, maji kutoka chemchemi ya maji ya uzima, bure.
Leave a Reply