Biblia inasema nini kuhusu hisia – Mistari yote ya Biblia kuhusu hisia

Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia hisia

Mithali 29 : 11
11 Mpumbavu hudhihirisha hasira yake yote; Bali mwenye hekima huizuia na kuituliza.

Wafilipi 4 : 6 – 7
6 Msijisumbue kwa neno lolote; bali katika kila neno kwa kusali na kuomba, pamoja na kushukuru, haja zenu na zijulikane na Mungu.
7 Na amani ya Mungu, ipitayo akili zote, itawahifadhi mioyo yenu na nia zenu katika Kristo Yesu.

Wafilipi 4 : 13
13 Nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu.

Mathayo 18 : 15 – 17
15 ④ Na ndugu yako akikukosea, nenda ukamwonye, wewe na yeye peke yenu; akikusikia, umempata nduguyo.
16 ⑤ La, kama hasikii, chukua pamoja nawe tena mtu mmoja au wawili, ili kwa vinywa vya mashahidi wawili au watatu kila neno lithibitike.
17 ⑥ Na asipowasikiliza wao, liambie kanisa; na asipolisikiliza kanisa pia, na awe kwako kama mtu wa mataifa na mtoza ushuru.

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *