Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia hasira
Zaburi 37 : 8
8 Ukomeshe hasira, uache ghadhabu, Usikasirike, mwisho wake ni kutenda mabaya.
Mithali 14 : 29
29 Asiye mwepesi wa hasira ana fahamu nyingi; Bali mwenye roho ya hamaki hutukuza upumbavu.
Yakobo 1 : 20
20 kwa maana hasira ya mwanadamu haiitendi haki ya Mungu.
Wagalatia 5 : 12
12 ⑦ Laiti hao wanaowatia mashaka wangejikata nafsi zao!
Waefeso 4 : 26
26 ⑬ Muwe na hasira, ila msitende dhambi; jua lisichwe na uchungu wenu bado haujawatoka;
Yakobo 1 : 19
19 Hayo mnajua, ndugu zangu wapenzi. Basi kila mtu na awe mwepesi wa kusikia, bali si mwepesi wa kusema; wala kukasirika;
Mithali 15 : 1
1 Jawabu la upole hugeuza hasira; Bali neno liumizalo huchochea ghadhabu.
Waefeso 4 : 31
31 ⑰ Uchungu wote na ghadhabu na hasira na kelele na matusi yaondoke kwenu, pamoja na kila namna ya ubaya;
Mithali 19 : 11
11 Busara ya mtu huiahirisha hasira yake; Nayo ni fahari yake kusamehe makosa.
Mhubiri 7 : 9
9 ② Usifanye haraka kukasirika rohoni mwako, Maana hasira hukaa kifuani mwa wapumbavu.
Yakobo 1 : 19 – 20
19 Hayo mnajua, ndugu zangu wapenzi. Basi kila mtu na awe mwepesi wa kusikia, bali si mwepesi wa kusema; wala kukasirika;
20 kwa maana hasira ya mwanadamu haiitendi haki ya Mungu.
Mithali 29 : 11
11 Mpumbavu hudhihirisha hasira yake yote; Bali mwenye hekima huizuia na kuituliza.
Mithali 16 : 32
32 Asiye mwepesi wa hasira ni mwema kuliko shujaa; Na mtu aitawalaye roho yake kuliko mtu atekaye mji.
Waefeso 4 : 26 – 27
26 ⑬ Muwe na hasira, ila msitende dhambi; jua lisichwe na uchungu wenu bado haujawatoka;
27 wala msimpe Ibilisi nafasi.
Wakolosai 3 : 8
8 Lakini sasa yawekeni mbali nanyi haya yote, hasira, na ghadhabu, na uovu, na masuto, na matusi vinywani mwenu.
Mithali 15 : 18
18 Mtu wa hasira huchochea ugomvi; Bali asiye mwepesi wa hasira hutuliza mashindano.
Zaburi 103 : 8
8 ⑥ BWANA amejaa huruma na neema, Haoni hasira upesi, ni mwingi wa fadhili.
Mathayo 5 : 22
22 ⑫ Bali mimi nawaambieni, Kila amkasirikiaye ndugu yake itampasa hukumu; na mtu akimtusi ndugu yake, anastahili kuhukumiwa na baraza; na mtu akimwambia nduguye, Ewe mpumbavu, anastahili kuingia katika moto wa Jehanamu.
1 Timotheo 2 : 8
8 Basi, nataka wanaume waombe kila mahali, huku wakiinua mikono iliyotakata pasipo hasira wala majadiliano.
Mithali 29 : 9
9 Mwenye hekima akijadiliana na mpumbavu; Akikasirika au akicheka, pia hapana raha.
Leave a Reply