Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia Fiziolojia
Ayubu 10 : 11
11 Umenivika ngozi na nyama, Na kuniunga pamoja kwa mifupa na mishipa.
Zaburi 139 : 16
16 Macho yako yaliniona kabla sijakamilika; Kitabuni mwako ziliandikwa zote pia, Siku zilizoamriwa kabla hazijawa bado.
Waefeso 4 : 16
16 ④ Katika yeye mwili wote ukiungamanishwa na kushikanishwa kwa msaada wa kila kiungo, kwa kadiri ya utendaji wa kila sehemu moja moja, huukuza mwili upate kujijenga wenyewe katika upendo.
Wakolosai 2 : 19
19 ⑳ wala hakishiki Kichwa, ambacho kwa yeye mwili wote ukineemeshwa na kuungamanishwa kwa viungo na mishipa, hukua kama atakavyo Mungu.
Leave a Reply