Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia Chuki
Zaburi 97 : 10
10 ⑯ Enyi mmpendao BWANA, uchukieni uovu; Huwalinda nafsi zao watauwa wake, Na kuwaokoa na mkono wa wasio haki.
Zaburi 101 : 3
3 Sitaweka mbele ya macho yangu Neno la uovu. Kazi yao waliopotoka naichukia, Haitaambatana nami.
Zaburi 119 : 104
104 Kwa mausia yako najipatia ufahamu, Ndiyo maana naichukia kila njia ya uongo.
Zaburi 119 : 128
128 Maana nayafuata mausia yako yote, kuwa ya adili, Kila njia ya uongo naichukia.
Zaburi 119 : 163
163 Nimeuchukia uongo, umenikirihi, Sheria yako nimeipenda.
Zaburi 139 : 22
22 Nawachukia kwa upepo wa chuki, Wamekuwa adui kwangu.
Zaburi 5 : 5
5 Wajivunao hawatasimama mbele za macho yako; Unawachukia wote watendao uovu.
Zaburi 45 : 7
7 ⑧ Umeipenda haki; Umeichukia dhuluma. Kwa hiyo MUNGU, Mungu wako, amekutia mafuta, Mafuta ya furaha kuliko wenzako.
Malaki 2 : 16
16 Maana mimi nakuchukia kuachana, asema BWANA, Mungu wa Israeli; naye aifunikizaye nguo yake kwa udhalimu namchukia, asema BWANA wa majeshi; basi jihadharini roho zenu, msije mkatenda kwa hiana.
Mambo ya Walawi 19 : 17
17 Usimchukie ndugu yako moyoni mwako; ni lazima kumkemea jirani yako, au ulipizwe uovu kwa ajili yake
Zaburi 25 : 19
19 Uwatazame adui zangu, maana ni wengi, Na kwa namna wanavyonichukia kwa ukatili mwingi.
Zaburi 35 : 19
19 ⑱ Walio adui zangu bure wasinisimange, Wanaonichukia bila sababu wasining’ong’e.
Mithali 10 : 12
12 ⑮ Kuchukiana huleta fitina; Bali kupendana husitiri makosa yote.
Mithali 10 : 18
18 Yeye afichaye chuki ana midomo ya uongo, Na yeye asingiziaye ni mpumbavu.
Mithali 15 : 17
17 Chakula cha mboga palipo na upendo; Ni bora kuliko ng’ombe aliyenona pamoja na kuchukiana.
Mithali 26 : 26
26 Ingawa chuki hufunikwa na hila; Uovu wake utadhihirika mbele ya kusanyiko.
Mathayo 5 : 44
44 lakini mimi nawaambia, Wapendeni adui zenu, waombeeni wanaowaudhi,
Mathayo 6 : 15
15 Bali msipowasamehe watu makosa yao, wala Baba yenu hatawasamehe ninyi makosa yenu.
Mathayo 10 : 22
22 Nanyi mtakuwa mkichukiwa na watu wote kwa ajili ya jina langu; lakini mwenye kuvumilia hata mwisho, ndiye atakayeokoka.
Yohana 15 : 19
19 Kama mngekuwa wa ulimwengu, ulimwengu ungewapenda walio wake; lakini kwa kuwa ninyi si wa ulimwengu, bali mimi niliwachagua katika ulimwengu, kwa sababu hiyo ulimwengu huwachukia.
Yohana 15 : 25
25 Lakini litimie lile neno lililoandikwa katika torati yao, Walinichukia bure.
Yohana 17 : 14
14 Mimi nimewapa neno lako; na ulimwengu umewachukia; kwa kuwa wao si wa ulimwengu, kama mimi nisivyo wa ulimwengu.
Wagalatia 5 : 20
20 ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, mafarakano, uzushi,
Waefeso 4 : 31
31 ⑰ Uchungu wote na ghadhabu na hasira na kelele na matusi yaondoke kwenu, pamoja na kila namna ya ubaya;
Wakolosai 3 : 8
8 Lakini sasa yawekeni mbali nanyi haya yote, hasira, na ghadhabu, na uovu, na masuto, na matusi vinywani mwenu.
Leave a Reply