Biblia inasema nini kuhusu Asali – Mistari yote ya Biblia kuhusu Asali

Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia Asali

Kutoka 16 : 31
31 ⑬ Na nyumba ya Israeli wakakiita jina lake Mana; nacho kilikuwa mfano wa chembe za mtama, nyeupe; na utamu wake ulikuwa kama utamu wa maandazi membamba yaliyoandaliwa kwa asali.

2 Samweli 17 : 29
29 ⑮ na asali, na siagi, na kondoo, na samli ya ng’ombe, wapate kula Daudi na watu waliokuwa pamoja naye; kwani walisema, Watu hao wanaona njaa, tena wamechoka, nao wana kiu huku nyikani.

Mithali 25 : 27
27 Haifai kula asali nyingi mno; Vile vile mtu kutafuta utukufu wake mwenyewe si utukufu.

Wimbo ulio Bora 4 : 11
11 ③ Bibi arusi, midomo yako yadondosha asali, Asali na maziwa viko chini ya ulimi wako; Na harufu ya mavazi yako Ni kama harufu ya Lebanoni.

Isaya 7 : 15
15 Siagi na asali atakula, wakati ajuapo kuyakataa mabaya na kuyachagua mema.

Mathayo 3 : 4
4 ⑥ Naye Yohana mwenyewe alikuwa na vazi lake la singa za ngamia, na mshipi wa ngozi kiunoni mwake; na chakula chake kilikuwa nzige na asali ya mwituni.

Luka 24 : 42
42 Wakampa kipande cha samaki wa kuokwa.

Mambo ya Walawi 2 : 11
11 Sadaka ya unga yoyote itakayosongezwa kwa BWANA isitiwe chachu kabisa; kwa kuwa hamtateketeza chachu, wala asali yoyote, kuwa ni sadaka ya kusongezwa kwa BWANA kwa njia ya moto.

Kumbukumbu la Torati 32 : 13
13 Alimpandisha mahali pa nchi palipoinuka, Naye akala mazao ya mashamba; Akamnyonyesha asali iliyotoka jabalini, Na mafuta yaliyotoka katika mwamba wa gumegume;

Zaburi 81 : 16
16 Naam, ningewalisha kwa ngano iliyo bora zaidi, Ningewashibisha kwa asali itokayo mwambani.

1 Samweli 14 : 25
25 Nao watu wote wakaingia mwituni; na humo mlikuwa na asali juu ya nchi.

Waamuzi 14 : 14
14 Naye akawaambia, Kutoka kwa huyo kikatoka chakula, Kutoka kwa huyo mwenye nguvu kikatoka kitamu. Nao katika siku tatu hawakuweza kukifumbua hicho kitendawili.

Mwanzo 43 : 11
11 Israeli, baba yao, akawaambia, Kama ndivyo, fanyeni hivi; twaeni tunu za nchi katika vyombo vyenu, mkamchukulie mtu huyo zawadi, zeri kidogo, na asali kidogo, ubani, na manemane, na jozi, na lozi.

Kutoka 3 : 8
8 ⑫ nami nimeshuka ili niwaokoe kutoka kwa mikono ya Wamisri, niwapandishe kutoka nchi ile, hadi nchi njema, kisha pana; nchi itiririkayo maziwa na asali; hata mahali pa Mkanaani, na Mhiti, na Mwamori, na Mperizi, na Mhivi, na Myebusi.

Mambo ya Walawi 20 : 24
24 ⑪ Lakini mimi nimewaambia ninyi, Mtairithi nchi yao, nami nitawapa ninyi kuimiliki; nchi iliyojaa maziwa na asali; mimi ni BWANA, Mungu wenu, niliyewatenga ninyi na mataifa.

Kumbukumbu la Torati 8 : 8
8 nchi ya ngano na shayiri, na mizabibu, na mitini, na mikomamanga; nchi ya mizeituni yenye mafuta, na asali;

Ezekieli 20 : 6
6 katika siku ile niliwainulia mkono wangu, kuwatoa katika nchi ya Misri, na kuwaingiza katika nchi niliyowapelelezea, itiririkayo maziwa na asali, ambayo ni utukufu wa nchi zote;

2 Wafalme 18 : 32
32 ⑰ hata nije nikawachukue mpaka nchi iliyo kama nchi yenu wenyewe, nchi ya nafaka na divai, nchi ya chakula na mashamba ya mizabibu, nchi ya mafuta ya mzeituni na asali, ili mpate kuishi, msife; wala msimsikilize Hezekia, awadanganyapo, akisema, BWANA atatuokoa.

Ezekieli 27 : 17
17 ③ Yuda, na nchi ya Israeli, walikuwa wachuuzi wako; walitoa badala ya bidhaa yako ngano ya Minithi, na mtama, na asali, na mafuta, na zeri.

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *