Biblia inasema nini kuhusu adui zetu – Mistari yote ya Biblia kuhusu adui zetu

Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia adui zetu

Mathayo 22 : 44
44 ⑤ Bwana alimwambia Bwana wangu, Uketi katika mkono wangu wa kulia, Hata niwawekapo adui zako Kuwa chini ya miguu yako?

Yohana 14 : 1
1 ③ Msifadhaike mioyoni mwenu; mnamwamini Mungu, niaminini na mimi.

2 Petro 2 : 1
1 Lakini kulitokea manabii wa uongo katika wale watu, kama vile kwenu kutakavyokuwako waalimu wa uongo, watakaoingiza kwa werevu uzushi wa kupoteza, wakimkana hata Bwana aliyewanunua, wakijiletea uharibifu usiokawia.

Mathayo 5 : 38 – 39
38 Mmesikia kwamba imenenwa, Jicho kwa jicho, na jino kwa jino;
39 Lakini mimi nawaambia, Msishindane na mtu mwovu; lakini mtu akupigaye shavu la kulia, mgeuzie na la pili.

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *