Biblia inasema nini kuhusu Abigaili – Mistari yote ya Biblia kuhusu Abigaili

Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia Abigaili

1 Samweli 27 : 3
3 Daudi akakaa huko Gathi pamoja na Akishi, yeye na watu wake, kila mtu na watu wa nyumbani mwake; Daudi naye alikuwa na wakeze wawili, Ahinoamu wa Yezreeli, na Abigaili wa Karmeli, aliyekuwa mkewe Nabali.

2 Samweli 2 : 2
2 Basi Daudi akapanda aende huko, pamoja na wakeze wawili, Ahinoamu wa Yezreeli, na Abigaili, mkewe Nabali, wa Karmeli.

2 Samweli 3 : 3
3 ⑫ na wa pili wake Danieli, wa Abigaili mkewe Nabali wa Karmeli; na wa tatu Absalomu, mwana wa Maaka binti Talmai, mfalme wa Geshuri,

1 Mambo ya Nyakati 3 : 1
1 Basi hawa ndio wana wa Daudi, aliozaliwa huko Hebroni; Amnoni, mzaliwa wa kwanza, mwana wa Ahinoamu, Myezreeli; wa pili, Danieli, wa Abigaili, Mkarmeli;

1 Samweli 30 : 18
18 Daudi akawapokonya wote waliokuwa wamechukuliwa na Waamaleki; naye Daudi akawaokoa wakeze wawili.

2 Samweli 17 : 25
25 Naye Absalomu akamweka Amasa awe juu ya jeshi mahali pa Yoabu. Basi huyo Amasa alikuwa mwana wa mtu, jina lake Yetheri, Mwishmaeli, aliyeingia kwa Abigali, binti Nahashi, nduguye Seruya, mamaye Yoabu.

1 Mambo ya Nyakati 2 : 17
17 ⑭ Na Abigaili akamzaa Amasa; na babaye Amasa ni Yetheri, Mwishmaeli.

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *