KUMWONA KRISTO KATIKA MAANDIKO YOTE

*Maandiko ya somo:* _Luka 24:27 wanafunzi wawili katika njia ya Emau, akawaeleza katika maandiko yote mambo yaliyomhusu yeye. Sio katika baadhi ya maandiko bali katika maandiko yote. Hii ina maana kwamba katika maandiko yote, yeye ndiye mtu mkuu anayezungumziwa. Yesu ndiye kiini cha yote. Kila unapofungua maandiko unaona nani na unaona nini? Wengine hufungua maandiko ili kuona kazi, wengine hufungua maandiko kuona mke, wengine hufungua maandiko kuona nyumba n.k. Hata hivyo mkuu kuliko wote ni yeye afunguaye maandiko na kumwona Kristo. Mara tu unapomwona Kristo ndipo utaona pia yote yanayokuhusu. Halujah utukufu kwa Mungu. Maandiko yanaposema kumtazama Yesu mwanzilishi na mwisho wa imani yetu, hii ina maana gani? Ina maana pale unapompoteza Kristo katika maandiko basi umefunikwa kwa kuwa yeye ndiye kitovu cha kila kitu na kiini cha yote. Hata wakati mambo yako hayaendi sawa, mara unapomuona Kristo, umeona amani, umeona uponyaji, umeona mafanikio ohhh utukufu kwa Mungu. *Jifunze zaidi* Waebrania 12:2 Yohana 5:39 *NUGGET* Tunapaswa kumuona Kristo katika maandiko yote, yeye ndiye maono makubwa sana ambayo unaweza kuwa nayo, yeye ndiye maono yanayoishi na kudumu milele, yeye ndiye maono ambayo itakaa daima moyoni mwako vizazi vyote milele na milele Amina. *Maombi* Baba katika jina la Yesu nakushukuru kwa zawadi kuu uliyotukirimia, zawadi ya mwanao Yesu Kristo, kila tunapofungua neno lako, tunayemuona ni yeye maana yeye ndiye amani, furaha yetu. upendo na mambo yote, Amina.

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *