Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia wivu
Kutoka 34 : 14
14 ⑯ Maana hutamwabudu mungu mwingine, kwa kuwa BWANA, ambaye jina lake ni mwenye wivu, ni Mungu mwenye wivu.
Mithali 14 : 30
30 Moyo ulio mzima ni uhai wa mwili; Bali husuda ni ubovu wa mifupa.
Mithali 23 : 17
17 Moyo wako usiwahusudu wenye dhambi; Bali mche BWANA mchana kutwa;
Wagalatia 5 : 19 – 21
19 ⑬ Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya, uasherati, uchafu, ufisadi,
20 ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, mafarakano, uzushi,
21 ⑭ husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo, katika hayo nawaambia mapema, kama nilivyokwisha kuwaambia, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu.
1 Petro 2 : 1
1 Basi, wekeni mbali uovu wote na hila yote, na unafiki na husuda na masingizio yote.
Wagalatia 5 : 26
26 ⑲ Tusijisifu bure, tukichokozana na kuhusudiana.
Mithali 24 : 1
1 Usiwawaonee wivu watu waovu, Wala usitamani kuwa pamoja nao;
Yakobo 3 : 16
16 Maana hapo palipo wivu na ugomvi ndipo palipo machafuko, na kila tendo baya.
1 Wakorintho 13 : 4
4 Upendo huvumilia, hufadhili; upendo hauhusudu; upendo hautakabari; haujivuni;
Tito 3 : 3
3 Maana hapo zamani sisi nasi tulikuwa hatuna akili, tulikuwa waasi, tumedanganywa, huku tukitumikia tamaa na anasa za namna nyingi, tukiishi katika uovu na husuda, tukichukiza na kuchukiana.
Marko 7 : 20 – 23
20 Akasema, Kimtokacho mtu ndicho kimtiacho unajisi.
21 Kwa maana ndani ya mioyo ya watu hutoka mawazo mabaya, uasherati,
22 wizi, uuaji, uzinzi, tamaa mbaya, ukorofi, hila, ufisadi, kijicho, matukano, kiburi, upumbavu.
23 Haya yote yaliyo maovu yatoka ndani, nayo yamtia mtu unajisi.
1 Timotheo 6 : 4
4 amejivuna; wala hafahamu neno lolote; bali ana wazimu wa kuwazia habari za maswali, na mashindano ya maneno, ambayo katika hayo hutoka husuda, na ugomvi, na matusi, na shuku mbaya;
Leave a Reply