Biblia inasema nini kuhusu wazee – Mistari yote ya Biblia kuhusu wazee

Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia wazee

1 Timotheo 5 : 1 – 2
1 Mzee usimkemee, bali umwonye kama baba; na wanaume vijana kama ndugu;
2 wanawake wazee kama mama; wanawake vijana kama ndugu wa kike; katika usafi wote.

Mambo ya Walawi 19 : 32
32 Mwondokeeni mtu mwenye mvi; heshimuni uso wa mtu mzee; nawe mche Mungu wako, Mimi ndimi BWANA.

Mithali 23 : 22
22 Msikilize baba yako aliyekuzaa, Wala usimdharau mama yako akiwa mzee.

Kutoka 20 : 12
12 Waheshimu baba yako na mama yako; siku zako zipate kuwa nyingi katika nchi upewayo na BWANA, Mungu wako.

Isaya 40 : 28 – 31
28 Je! Wewe hukujua? Hukusikia? Yeye Mungu wa milele, BWANA, Muumba miisho ya dunia, hazimii, wala hachoki; akili zake hazichunguziki.
29 Huwapa nguvu wazimiao, humwongezea nguvu yeye asiyekuwa na uwezo.
30 Hata vijana watazimia na kuchoka, na vijana wanaume wataanguka;
31 bali wao wamngojeao BWANA watapata nguvu mpya; watapanda juu kwa mbawa kama tai; watakimbia, wala hawatachoka; watakwenda kwa miguu, wala hawatazimia.

Mithali 20 : 29
29 Fahari ya vijana ni nguvu zao, Na uzuri wa wazee ni kichwa chenye mvi.

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *