Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia Uvivu
Mithali 6 : 6
6 Ewe mvivu, mwendee chungu, Zitafakari njia zake ukapate hekima.
Mithali 6 : 11
11 Hivyo umaskini wako huja kama mnyang’anyi, Na uhitaji wako kama mtu mwenye silaha.
Mithali 10 : 5
5 Akusanyaye wakati wa joto ni mwana mwenye hekima; Bali asinziaye wakati wa mavuno ni mwana mwenye kuaibisha.
Mithali 10 : 26
26 Kama siki menoni, na kama moshi machoni, Ndivyo alivyo mtu mvivu kwa hao waliomwajiri.
Mithali 12 : 9
9 Afadhali mtu anayedharauliwa, ikiwa ana mtumwa, Kuliko ajisifuye, ikiwa anahitaji chakula.
Mithali 12 : 24
24 ⑥ Mkono wa mwenye bidii utatawala; Bali mvivu atalipishwa kodi.
Mithali 12 : 27
27 Mtu mvivu hapiki mawindo yake; Bali mwenye bidii anazo mali za thamani.
Mithali 13 : 4
4 Nafsi ya mtu mvivu hutamani asipate kitu; Bali nafsi ya mwenye bidii itanenepeshwa.
Mithali 14 : 23
23 Katika kila kazi mna faida; Bali maneno ya midomo huleta hasara tu.
Mithali 15 : 19
19 Njia ya mtu mvivu ni kama boma la miiba; Bali mapito yao wenye unyofu hufanyika njia kuu.
Mithali 18 : 9
9 Yeye naye aliye mvivu katika kazi yake, Ni ndugu yake aliye mharibifu.
Mithali 19 : 15
15 Uvivu humtia mtu katika usingizi mzito; Na nafsi yake mvivu itaona njaa.
Mithali 19 : 24
24 Mtu mvivu hutia mkono wake katika sahani; Wala hataki hata kuupeleka kinywani pake.
Mithali 20 : 4
4 Mtu mvivu hataki kulima wakati wa baridi; Hivyo wakati wa mavuno ataomba, hana kitu.
Mithali 20 : 13
13 ⑩ Usipende usingizi usije ukawa maskini; Fumbua macho yako nawe utashiba chakula.
Mithali 21 : 25
25 Matakwa yake mtu mvivu humwua, Kwa maana mikono yake hukataa kufanya kazi.
Mithali 23 : 21
21 Kwa maana mlevi na mlafi huingia umaskini, Na utepetevu humvika mtu nguo mbovu.
Mithali 24 : 31
31 ⑧ Kumbe! Lote pia limemea miiba; Uso wake ulifunikwa kwa viwawi; Na ukuta wake wa mawe umebomoka.
Mithali 24 : 34
34 Hivyo, umaskini wako huja kama mnyang’anyi, Na uhitaji wako kama mtu mwenye silaha.
Mithali 26 : 16
16 Mtu mvivu ni mwenye hekima machoni pake, Kuliko watu saba wawezao kutoa sababu.
Mithali 22 : 13
13 Mtu mvivu husema, Simba yuko nje; Nitauawa katika njia kuu.
Mhubiri 4 : 5
5 Mpumbavu huikunja mikono yake, Naye hula chakula chake mwenyewe;
Mhubiri 10 : 18
18 Kwa sababu ya uvivu paa hunepa; Na kwa ulegevu wa mikono nyumba huvuja.
Isaya 56 : 10
10 Walinzi wake ni vipofu, wote pia hawana maarifa; wote ni mbwa walio bubu, hawawezi kulia; huota ndoto, hulala, hupenda usingizi.
Ezekieli 16 : 49
49 ⑮ Tazama, uovu wa dada yako, Sodoma, ulikuwa huu; kiburi, na kushiba chakula, na kufanikiwa, hayo yalikuwa ndani yake na binti zake; lakini hukuwasaidia maskini na wahitaji.
Luka 19 : 25
25 Wakamwambia, Bwana, anayo mafungu kumi.
Mathayo 20 : 7
7 Wakamwambia, Kwa sababu hakuna mtu aliyetuajiri. Akawaambia, nanyi pia nendeni katika shamba la mizabibu.
Leave a Reply