Biblia inasema nini kuhusu utulivu – Mistari yote ya Biblia kuhusu utulivu

Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia utulivu

Zaburi 46 : 10
10 ⑰ Tulieni, mjue ya kuwa Mimi ni Mungu, Nitakuzwa katika mataifa, nitakuzwa katika nchi.

Kutoka 14 : 14
14 ⑦ BWANA atawapigania ninyi, nanyi mtanyamaza kimya.

Kutoka 14 : 13
13 ⑥ Musa akawaambia watu, Msiogope, simameni tu, mkauone wokovu wa BWANA atakaowafanyia leo; kwa maana hao Wamisri mliowaona leo hamtawaona tena milele.

Ruthu 2 : 12
12 BWANA akujaze kwa kazi yako, nawe upewe thawabu kamili na BWANA, Mungu wa Israeli, ambaye umekuja kukimbilia chini ya mabawa yake.

Hesabu 9 : 8
8 Musa akawaambia, Ngojeni hapo; hata nipate sikiza BWANA atakaloagiza juu yenu.

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *