Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia Utulivu
1 Petro 1 : 13
13 Kwa hiyo iweni tayari, na makini;[1] mkiitumainia kwa utimilifu ile neema mtakayoletewa katika ufunuo wake Yesu Kristo.
1 Petro 5 : 8
8 ⑲ Muwe na kiasi na kukesha; kwa kuwa mshitaki wenu Ibilisi, kama simba angurumaye, huzunguka zunguka, akitafuta mtu ammeze.
Tito 2 : 12
12 nayo yatufundisha kukataa ubaya na tamaa za kidunia; tupate kuishi kwa kiasi, na haki, na utauwa, katika ulimwengu huu wa sasa;
1 Wathesalonike 5 : 6
6 Basi tusilale usingizi kama wengine, bali tukeshe, na kuwa na kiasi.
1 Petro 4 : 7
7 Lakini mwisho wa mambo yote umekaribia; basi, iweni na akili, mkeshe katika sala.
1 Timotheo 3 : 3
3 asiwe mtu wa kulewa, asiye dhalimu; bali awe mpole; asiwe mbishi, wala asiwe mwenye kupenda fedha;
Tito 1 : 8
8 bali awe mkarimu, mpenda wema, mwenye kiasi, mwenye haki, mtakatifu, mwenye kudhibiti nafsi yake;
1 Timotheo 3 : 11
11 ⑧ Vivyo hivyo wake zao na wawe wastahivu; wasiwe wachongezi; ila wawe watu wa kiasi, waaminifu katika mambo yote.
Tito 2 : 2
2 ya kwamba wazee wawe wenye kiasi, wastahivu, wenye busara, wazima katika imani na katika upendo na katika subira.
Tito 2 : 6
6 Vivyo hivyo na vijana waume uwaonye kuwa na kiasi;
Tito 2 : 4
4 ili wawatie wanawake vijana akili, wawapende waume zao, na kuwapenda watoto wao;
1 Wathesalonike 5 : 6
6 Basi tusilale usingizi kama wengine, bali tukeshe, na kuwa na kiasi.
1 Wathesalonike 5 : 8
8 Lakini sisi tulio wa mchana, tuwe na kiasi, hali tukijivika kifuani imani na upendo, na chapeo yetu iwe tumaini la wokovu.
1 Timotheo 2 : 9
9 Vivyo hivyo wanawake na wajipambe kwa mavazi ya kujisitiri, pamoja na adabu nzuri, na moyo wa kiasi; si kwa kusuka nywele, wala kwa dhahabu na lulu, wala kwa nguo za thamani;
Warumi 12 : 3
3 Kwa maana kwa neema niliyopewa namwambia kila mtu aliyeko kwenu asinuie makuu kupita ilivyompasa kunuia; bali awe na nia ya kiasi, kama Mungu alivyomgawia kila mtu kiasi cha imani.
Tito 2 : 12
12 nayo yatufundisha kukataa ubaya na tamaa za kidunia; tupate kuishi kwa kiasi, na haki, na utauwa, katika ulimwengu huu wa sasa;
1 Petro 4 : 7
7 Lakini mwisho wa mambo yote umekaribia; basi, iweni na akili, mkeshe katika sala.
1 Petro 5 : 8
8 ⑲ Muwe na kiasi na kukesha; kwa kuwa mshitaki wenu Ibilisi, kama simba angurumaye, huzunguka zunguka, akitafuta mtu ammeze.
Leave a Reply