Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia Utekaji nyara
Kutoka 21 : 16
16 Yeye amwibaye mtu, na kumwuza, au akipatikana mkononi mwake, sharti atauawa huyo.
Kumbukumbu la Torati 24 : 7
7 ⑥ Mtu akionekana anamwiba nduguze mmojawapo katika wana wa Israeli, akamfanya kama mtumwa, au kumwuza; na afe mwizi huyo; ndivyo utakavyoondoa uovu katikati yako.
Waamuzi 21 : 23
23 ⑩ Wana wa Benyamini wakafanya hivyo, wakajitwalia wake, kulingana na hesabu yao, katika hao waliocheza, wakawachukua wakaenda nao; kisha wakaenda kuurudia urithi wao, na kuijenga miji na kuishi humo.
Leave a Reply