Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia usikivu
Mhubiri 7 : 21
21 Tena, usitie moyoni mwako maneno yote wasemayo watu; usije ukamsikia mtumishi wako mwenyewe akikutukana.
Waefeso 4 : 31 – 32
31 ⑰ Uchungu wote na ghadhabu na hasira na kelele na matusi yaondoke kwenu, pamoja na kila namna ya ubaya;
32 ⑱ tena iweni wafadhili ninyi kwa ninyi, wenye huruma, mkasameheane kama Mungu katika Kristo alivyowasamehe ninyi.
Luka 12 : 3
3 Basi, yoyote mliyosema gizani yatasikiwa mwangani; na mliyonena sikioni mwa mtu katika vyumba vya ndani, yatatangazwa juu ya dari.
2 Wathesalonike 2 : 11
11 Kwa hiyo Mungu anawaletea upotevu mwingi, wauamini uongo;
Waraka kwa Waebrania 4 : 15
15 Kwa kuwa hamna kuhani mkuu asiyeweza kuchukuana nasi katika mambo yetu ya udhaifu; bali yeye alijaribiwa kama sisi katika mambo yote, bila kufanya dhambi.
Leave a Reply