Biblia inasema nini kuhusu Ushuhuda – Mistari yote ya Biblia kuhusu Ushuhuda

Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia Ushuhuda

1 Mambo ya Nyakati 16 : 9
9 Mwimbieni, mwimbieni nyimbo za kumsifu; Yatangazeni matendo yake yote ya ajabu.

Zaburi 9 : 11
11 Mwimbieni BWANA akaaye Sayuni, Yatangazeni kwa watu matendo yake.

Zaburi 18 : 49
49 Basi, BWANA, nitakushukuru kati ya mataifa, Nami nitaliimbia jina lako.

Zaburi 26 : 7
7 Ili niitangaze sauti ya kushukuru, Na kuzisimulia kazi zako za ajabu.

Zaburi 119 : 27
27 Unifahamishe njia ya maagizo yako, Nami nitayatafakari maajabu yako.

Zaburi 119 : 172
172 Ulimi wangu na uiimbe ahadi yako, Maana maagizo yako yote ni ya haki.

Zaburi 145 : 12
12 Ili kuwajulisha watu matendo yake makuu, Na utukufu wa fahari ya ufalme wake.

Isaya 12 : 6
6 Paza sauti, piga kelele, mwenyeji wa Sayuni; Maana Mtakatifu wa Israeli ni mkuu kati yako.

Isaya 32 : 4
4 Tena moyo wa mtu mwenye hamaki utafahamu maarifa, na ndimi zao wenye kigugumizi zitakuwa tayari kunena sawasawa.

Isaya 43 : 10
10 Ninyi ni mashahidi wangu, asema BWANA, na mtumishi niliyemchagua; mpate kujua, na kuniamini, na kufahamu ya kuwa mimi ndiye; kabla yangu hakuumbwa Mungu awaye yote, wala baada yangu mimi hatakuwapo mwingine.

Isaya 44 : 8
8 ② Msiogope wala msifanye hofu; je! Sikukuambia haya zamani na kuyatangaza? Na ninyi ni mashahidi wangu. Je! Yuko Mungu zaidi yangu mimi? Hakika hapana Mwamba; mimi sijui mwingine.

Isaya 45 : 24
24 Mmoja ataniambia, Kwa BWANA, peke yake, iko haki na nguvu; naam, watu watamwendea yeye, na wote waliomkasirikia watatahayarika.

Yeremia 51 : 10
10 ④ BWANA ameitokeza haki yetu; Njooni, tutangaze katika Sayuni Habari za kazi ya BWANA, Mungu wetu.

Marko 4 : 21
21 Akawaambia, Mwaonaje? Taa huja ili kuwekwa chini ya pishi, au mvunguni? Si kuwekwa juu ya kiango?

Mathayo 5 : 15
15 ⑤ Wala watu hawawashi taa na kuiweka chini ya pishi, bali juu ya kiango; nayo yawaangaza wote waliomo nyumbani.

Luka 8 : 16
16 Hakuna mtu ambaye akiisha washa taa huifunika kwa mtungi, au kuiweka mvunguni, bali huiweka juu ya kiango, ili waingiao wapate kuona nuru yake.

Marko 5 : 16
16 Na wale waliokuwa wameona waliwaeleza ni mambo gani yaliyompata yule mwenye pepo, na kuhusu nguruwe.

Marko 5 : 20
20 Akaenda zake, akaanza kuhubiri katika Dekapoli, ni mambo gani makuu Yesu aliyomtendea; watu wote wakastaajabu.

Luka 8 : 39
39 Rudi nyumbani kwako, ukahubiri yalivyo makuu Mungu aliyokutendea. Akaenda zake, akihubiri katika mji wote, yalivyo makuu mambo aliyotendewa na Yesu.

Luka 12 : 9
9 na mwenye kunikana mbele ya watu, huyo atakanwa mbele ya malaika wa Mungu.

Mathayo 10 : 32
32 Basi, kila mtu atakayenikiri mbele ya watu, nami nitamkiri mbele za Baba yangu aliye mbinguni.

Luka 24 : 48
48 Nanyi ndinyi mashahidi wa mambo haya.

Yohana 4 : 30
30 Basi wakatoka mjini, wakamwendea.

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *