Biblia inasema nini kuhusu Ushirika wa Kikristo – Mistari yote ya Biblia kuhusu Ushirika wa Kikristo

Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia Ushirika wa Kikristo

Waraka kwa Waebrania 10 : 24 – 25
24 ⑪ tukaangaliane sisi kwa sisi na kuhimizana katika upendo na kazi nzuri;
25 ⑫ wala tusiache kukusanyika pamoja, kama ilivyo desturi ya wengine; bali tuonyane; na kuzidi kufanya hivyo, kwa kadiri muonavyo siku ile kuwa inakaribia.

Matendo 2 : 42
42 ⑳ Wakawa wakidumu katika fundisho la mitume, na katika ushirika, na katika kuumega mkate, na katika kusali.

Warumi 12 : 10
10 Kwa pendo la udugu, mpendane ninyi kwa ninyi; kwa heshima mkiwatanguliza wenzenu;

1 Yohana 1 : 7
7 bali tukienenda katika nuru, kama yeye alivyo katika nuru, tunashirikiana sisi kwa sisi, na damu yake Yesu, Mwana wake, yatusafisha dhambi yote.

1 Wakorintho 12 : 12
12 Maana kama vile mwili ni mmoja, nao una viungo vingi, na viungo vyote vya mwili ule, navyo ni vingi, ni mwili mmoja; vivyo hivyo na Kristo.

1 Yohana 4 : 11
11 Wapenzi ikiwa Mungu alitupenda sisi hivi, imetupasa na sisi kupendana.

1 Yohana 1 : 3
3 hilo tuliloliona na kulisikia, tunawahubiria na ninyi; ili nanyi pia mpate kushirikiana nasi: na ushirika wetu ni pamoja na Baba, na pamoja na Mwana wake Yesu Kristo.

1 Petro 4 : 9
9 ① Mkaribishane ninyi kwa ninyi, pasipo kunung’unika;

1 Petro 3 : 15
15 Muwe tayari siku zote kumjibu kila mtu awaulizaye habari za tumaini lililo ndani yenu; lakini kwa upole na kwa heshima.

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *