Biblia inasema nini kuhusu Usaliti – Mistari yote ya Biblia kuhusu Usaliti

Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia Usaliti

Mathayo 26 : 16
16 Tokea wakati huo akawa akitafuta nafasi apate kumsaliti.

Mathayo 26 : 50
50 Yesu akamwambia, Rafiki, fanya ulilolijia. Wakaenda, wakanyosha mikono yao wakamkamata Yesu.

Marko 14 : 11
11 Nao waliposikia walifurahi, wakaahidi kumpa fedha. Akatafuta njia ya kumsaliti wakati wa kufaa.

Luka 22 : 6
6 Akakubali, akatafuta nafasi ya kumsaliti kwao pasipokuwapo mkutano.

Luka 22 : 48
48 Yesu akamwambia, Yuda, wamsaliti Mwana wa Adamu kwa kumbusu?

Yohana 13 : 21
21 Naye alipokwisha kusema hayo, Yesu alifadhaika rohoni, akashuhudia akisema, Amin, amin, nawaambieni, Mmoja wenu atanisaliti.

Mathayo 20 : 18
18 Angalieni, tunapanda kwenda Yerusalemu; na Mwana wa Adamu atatiwa mikononi mwa wakuu wa makuhani na waandishi; nao watamhukumu afe;

Mathayo 24 : 10
10 Ndipo wengi watakapojikwaa, nao watasalitiana, na kuchukiana.

1 Samweli 22 : 10
10 Naye akamwuliza BWANA kwa ajili yake, akampa vyakula, akampa na ule upanga wa Goliathi, Mfilisti.

1 Samweli 21 : 10
10 Basi Daudi akaondoka, akakimbia siku ile, kwa hofu ya Sauli, akamwendea Akishi, mfalme wa Gathi.

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *