Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia Usafi
Kutoka 20 : 14
14 Usizini.
Ayubu 31 : 1
1 Nilifanya agano na macho yangu; Basi ningewezaje kumwangalia msichana?
Mithali 2 : 11
11 Busara itakulinda; Ufahamu utakuhifadhi.
Mithali 2 : 22
22 Bali waovu watatengwa na nchi, Nao wafanyao hila watang’olewa.
Mithali 5 : 21
21 Kwa maana njia za mwanadamu ziko mbele ya macho ya BWANA, Na mienendo yake yote huitafakari.
Mithali 6 : 25
25 ⑪ Usiutamani uzuri wake moyoni mwako; Wala usikubali akunase kwa kope za macho yake.
Mithali 7 : 5
5 Wapate kukulinda na malaya, Na mwasherati akubembelezaye kwa maneno yake.
Mithali 31 : 3
3 Usiwape wanawake nguvu zako; Wala moyo wako usiwape wale wanaowaharibu wafalme.
Mathayo 5 : 28
28 ⑯ lakini mimi nawaambia, Kila mtu atazamaye mwanamke kwa kumtamani, amekwisha kuzini naye moyoni mwake.
Matendo 15 : 20
20 bali tuwaandikie kwamba wajiepushe na unajisi wa sanamu, na uasherati, na nyama zilizosongolewa, na damu.
Warumi 13 : 13
13 ⑧ Kama ilivyohusika na mchana na tuenende kwa adabu; si kwa ulafi na ulevi, si kwa ufisadi na uasherati, si kwa ugomvi na wivu.
1 Wakorintho 6 : 19
19 ⑲ Au hamjui ya kuwa mwili wenu ni hekalu la Roho Mtakatifu aliye ndani yenu, mliyepewa na Mungu? Wala ninyi si mali yenu wenyewe;
1 Wakorintho 7 : 2
2 Lakini kwa sababu ya zinaa kila mwanamume na awe na mke wake mwenyewe, na kila mwanamke na awe na mume wake mwenyewe.
1 Wakorintho 7 : 9
9 Lakini ikiwa hawawezi kujizuia, na waoe; maana ni afadhali kuoa kuliko kuwaka tamaa.
1 Wakorintho 7 : 26
26 Basi, naona hili kuwa jema, kwa ajili ya shida iliyopo, kwamba ni vema mtu akae kama alivyo.
1 Wakorintho 7 : 37
37 Lakini yeye aliyesimama kwa uthabiti wa moyo wake, hana sharti, lakini aweza kuyatawala mapenzi yake, tena amekusudia moyoni mwake kumlinda mwanamwali wake, atatenda vema.
Waefeso 5 : 3
3 Lakini uasherati usitajwe kwenu kamwe, wala uchafu wowote wa kutamani, kama iwastahilivyo watakatifu;
Wakolosai 3 : 5
5 Basi, viueni viungo vyenu vilivyo vya kidunia, uasherati, uchafu, tamaa mbaya, mawazo mabaya, na kutamani, ndiyo ibada ya sanamu;
1 Wathesalonike 4 : 3
3 ⑧ Maana haya ndiyo mapenzi ya Mungu, kutakaswa kwenu, mwepukane na uasherati;
1 Wathesalonike 4 : 7
7 ⑬ Maana Mungu hakutuitia uchafu, bali tuwe katika utakaso.
Mwanzo 39 : 20
20 ⑤ Bwana wake akamtwaa Yusufu, akamtia gerezani, mahali wafungwa wa mfalme walimokuwa wamefungiwa, naye akawa humo gerezani.
Ruthu 3 : 13
13 ⑦ Wewe ungoje usiku huu; kisha, asubuhi, kama akikubali kukufanyia impasavyo jamaa, haya, na akufanyie; lakini ikiwa hataki yeye, basi mimi nitakufanyia impasavyo jamaa; BWANA aishivyo. Ulale wewe hadi asubuhi.
Leave a Reply