Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia Umwagiliaji
Kumbukumbu la Torati 11 : 10
10 ⑳ Kwa kuwa nchi mwingiayo kuimiliki, si mfano wa nchi ya Misri mlikotoka, uliyokuwa ukipanda mbegu zako humo na kuinyunyizia maji kwa mguu wako, kama shamba la mboga;
Mithali 21 : 1
1 Moyo wa mfalme huwa katika mkono wa BWANA; Kama mifereji ya maji huugeuza popote apendapo.
Mhubiri 2 : 6
6 nikajifanyia mabwawa ya maji, ya kuunyweshea msitu mlimopandwa miti michanga.
Isaya 58 : 11
11 Naye BWANA atakuongoza daima, ataishibisha nafsi yako mahali pasipokuwa na maji, na kuitia nguvu mifupa yako; nawe utakuwa kama bustani iliyotiwa maji, na kama chemchemi ambayo maji yake hayapungui.
1 Wakorintho 3 : 6
6 ⑰ Mimi nilipanda, Apolo akatia maji; bali mwenye kukuza ni Mungu.
1 Wakorintho 3 : 8
8 Basi yeye apandaye, na yeye atiaye maji ni wamoja, lakini kila mtu atapata thawabu yake mwenyewe kulingana na taabu yake mwenyewe.
Leave a Reply