Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia umoja
1 Petro 4 : 8
8 Zaidi ya yote iweni na bidii kubwa katika kupendana; kwa sababu upendano husitiri wingi wa dhambi.
Mhubiri 4 : 9
9 Afadhali kuwa wawili kuliko mmoja; Kwa sababu wana tuzo njema kwa kazi yao.
Yohana 13 : 34
34 Amri mpya nawapa, Mpendane. Kama vile nilivyowapenda ninyi, nanyi mpendane vivyo hivyo.
Zaburi 95 : 6
6 ③ Njoni, tuabudu, tusujudu, Tupige magoti mbele za BWANA aliyetuumba.
Wafilipi 2 : 2
2 ijalizeni furaha yangu, ili muwe na nia moja, wenye mapenzi mamoja, wenye roho moja, mkiwaza mamoja.
Leave a Reply