Biblia inasema nini kuhusu udanganyifu – Mistari yote ya Biblia kuhusu udanganyifu

Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia udanganyifu

Mithali 20 : 17
17 Chakula cha uongo ni kitamu kwa mtu; Lakini halafu kinywa chake kitajaa changarawe.

Mithali 6 : 16 – 19
16 Kuna vitu sita anavyovichukia BWANA; Naam, viko saba vilivyo chukizo kwake.
17 ⑤ Macho ya kiburi, ulimi wa uongo, Na mikono imwagayo damu isiyo na hatia;
18 ⑥ Moyo uwazao mawazo mabaya; Miguu iliyo myepesi kukimbilia maovu;
19 ⑦ Shahidi wa uongo asemaye uongo; Naye apandaye mbegu za fitina kati ya ndugu.

Zaburi 101 : 7
7 Hatakaa ndani ya nyumba yangu Mtu atendaye hila. Asemaye uongo hatathibitika Mbele ya macho yangu.

Mithali 26 : 24 – 26
24 Achukiaye huficha chuki kwa midomo yake; Naye huweka akiba ya hila moyoni mwake.
25 Anenapo maneno mazuri usimsadiki; Kwa maana ana machukizo saba moyoni mwake.
26 Ingawa chuki hufunikwa na hila; Uovu wake utadhihirika mbele ya kusanyiko.

Zaburi 120 : 2
2 Ee BWANA, uniponye Na midomo ya uongo na ulimi wa hila.

Zaburi 36 : 3
3 Maneno ya kinywa chake ni uovu na hila, Ameacha kuwa na akili na kutenda mema.

Warumi 16 : 18
18 ⑪ Kwa sababu walio hivyo hawamtumikii Bwana wetu Kristo, bali matumbo yao wenyewe; na kwa maneno laini na ya kujipendekeza waidanganya mioyo ya watu wanyofu.

Yeremia 17 : 9
9 Moyo huwa mdanganyifu kuliko vitu vyote, una ugonjwa wa kufisha; nani awezaye kuujua?

Wakolosai 2 : 8
8 ⑩ Angalieni mtu asiwafanye mateka kwa elimu yake ya bure na madanganyo matupu, kwa jinsi ya mapokeo ya wanadamu, kwa jinsi ya mafundisho ya awali ya ulimwengu, wala si kwa jinsi ya Kristo.

Zaburi 43 : 1
1 Ee Bwana, unihukumu, unitetee kwa taifa lisilo haki, Uniokoe kutoka kwa mtu wa hila asiye haki.

Mithali 19 : 9
9 Shahidi wa uongo hakosi ataadhibiwa; Naye asemaye uongo ataangamia.

Marko 7 : 20 – 23
20 Akasema, Kimtokacho mtu ndicho kimtiacho unajisi.
21 Kwa maana ndani ya mioyo ya watu hutoka mawazo mabaya, uasherati,
22 wizi, uuaji, uzinzi, tamaa mbaya, ukorofi, hila, ufisadi, kijicho, matukano, kiburi, upumbavu.
23 Haya yote yaliyo maovu yatoka ndani, nayo yamtia mtu unajisi.

Zaburi 10 : 7
7 Kinywa chake kimejaa laana, Na hila na dhuluma. Chini ya ulimi wake kuna madhara na uovu,

Yeremia 9 : 6
6 ⑥ Makao yako ya katikati ya hadaa; kwa hadaa wanakataa kunijua mimi, asema BWANA.

2 Timotheo 3 : 12 – 15
12 ⑰ Naam, na wote wapendao kuishi maisha ya utauwa katika Kristo Yesu wataudhiwa.
13 ⑱ Lakini watu waovu na wadanganyaji wataendelea, na kuzidi kuwa waovu, wakidanganya na kudanganyika.
14 ⑲ Bali wewe ukae katika mambo yale uliyofundishwa na kuhakikishwa, kwa maana unajua ni akina nani ambao ulijifunza kwao;
15 ⑳ na ya kuwa tangu utotoni umeyajua Maandiko Matakatifu, ambayo yaweza kukuhekimisha hata upate wokovu kwa imani iliyo katika Kristo Yesu.

Wakolosai 3 : 9 – 10
9 Msiambiane uongo, kwa kuwa mmevua kabisa utu wa kale, pamoja na matendo yake;
10 mkivaa utu mpya, unaofanywa upya katika ufahamu kulingana na mfano wake yeye aliyeuumba.

2 Timotheo 3 : 13
13 ⑱ Lakini watu waovu na wadanganyaji wataendelea, na kuzidi kuwa waovu, wakidanganya na kudanganyika.

1 Petro 2 : 1
1 Basi, wekeni mbali uovu wote na hila yote, na unafiki na husuda na masingizio yote.

Ufunuo 21 : 8
8 ⑥ Bali waoga, na wasioamini, na wachukizao, na wauaji, na wazinzi, na wachawi, na hao waabuduo sanamu, na waongo wote, sehemu yao ni katika lile ziwa liwakalo moto na kiberiti. Hii ndiyo mauti ya pili.

1 Petro 3 : 10
10 Kwa maana, Atakaye kupenda maisha, Na kuona siku njema, Auzuie ulimi wake usinene mabaya, Na midomo yake isiseme uongo.

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *