Biblia inasema nini kuhusu Tai – Mistari yote ya Biblia kuhusu Tai

Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia Tai

Mambo ya Walawi 11 : 13
13 ⑥ Kisha katika ndege hawa watakuwa ni machukizo kwenu; hawataliwa, ndio machukizo; tai, na furukombe, na kipungu;

Kumbukumbu la Torati 14 : 12
12 Lakini hawa msiwale; tai, na furukombe, na kipungu;

Kumbukumbu la Torati 28 : 49
49 ③ BWANA atakuletea taifa juu yako kutoka mbali, kutoka ncha ya dunia, kama arukavyo tai; taifa usiloufahamu ulimi wake;

Ayubu 9 : 26
26 Zimepita kama merikebu ziendazo mbio; Mfano wa tai ayashukiaye mawindo.

Mithali 30 : 19
19 Mwendo wa tai katika hewa; Na mwendo wa nyoka juu ya mwamba; Mwendo wa merikebu katikati ya bahari; Na mwendo wa mtu pamoja na msichana.

Yeremia 4 : 13
13 Tazama atapanda juu kama mawingu, na magari yake ya vita yatakuwa kama kisulisuli; farasi wake ni wepesi kuliko tai. Ole wetu, kwa sababu tumeharibika.

Yeremia 49 : 22
22 Tazama, atapanda na kuruka kama tai, na kutandaza mabawa yake juu ya Bozra; na mioyo ya mashujaa wa Edomu siku hiyo itakuwa kama moyo wa mwanamke akiwa katika uchungu wa kujifungua.

Maombolezo 4 : 19
19 Waliotufuatia ni wepesi Kuliko tai za mbinguni; Hao walitufuatia milimani, Nao walituotea jangwani.

Kumbukumbu la Torati 32 : 11
11 Mfano wa tai ataharikishaye kioto chake; Na kupapatika juu ya makinda yake, Alikunjua mbawa zake, akawatwaa, Akawachukua juu ya mbawa zake;

Ayubu 39 : 30
30 ⑰ Makinda yake nayo hufyonza damu; Na pale iliko mizoga ndiko aliko.

Yeremia 49 : 16
16 Kuhusu kuogofya kwako, Kiburi cha moyo wako kimekudanganya, Wewe ukaaye katika pango za majabali, Ushikaye kilele cha milima; Ujapofanya kiota chako juu sana kama tai, Nitakushusha kutoka huko; asema BWANA.

Kutoka 19 : 4
4 Mmeona jinsi nilivyowatendea Wamisri, na jinsi nilivyowachukua ninyi juu ya mbawa za tai, nikawaleta ninyi kwangu mimi.

Kumbukumbu la Torati 32 : 11
11 Mfano wa tai ataharikishaye kioto chake; Na kupapatika juu ya makinda yake, Alikunjua mbawa zake, akawatwaa, Akawachukua juu ya mbawa zake;

Zaburi 103 : 5
5 Aushibisha mema uzee wako, Ujana wako ukarejezwa kama tai;

Mika 1 : 16
16 Jinyoeni upara, jikateni nywele zenu, Kwa ajili ya watoto waliowafurahisha; Panueni upara wenu kama tai; Kwa maana wamekwenda mbali nanyi uhamishoni.

Mambo ya Walawi 11 : 18
18 ⑦ na mumbi, na mwari, na mderi;

Kutoka 19 : 4
4 Mmeona jinsi nilivyowatendea Wamisri, na jinsi nilivyowachukua ninyi juu ya mbawa za tai, nikawaleta ninyi kwangu mimi.

Kumbukumbu la Torati 32 : 11
11 Mfano wa tai ataharikishaye kioto chake; Na kupapatika juu ya makinda yake, Alikunjua mbawa zake, akawatwaa, Akawachukua juu ya mbawa zake;

Yeremia 48 : 40
40 ⑬ Maana BWANA asema hivi, Tazama, ataruka kama tai, na kutandaza mabawa yake juu ya Moabu.

Hosea 8 : 1
1 Tia baragumu kinywani mwako. Kama tai, anakuja juu ya nyumba ya BWANA; kwa sababu wamelivunja agano langu, wameiasi sheria yangu.

Ezekieli 1 : 10
10 Kwa habari za mfano wa nyuso zao; walikuwa na uso wa mwanadamu; na hao wanne walikuwa na uso wa simba upande wa kulia; na hao wanne walikuwa na uso wa ng’ombe upande wa kushoto; na hao wanne walikuwa na uso wa tai pia.

Ezekieli 10 : 14
14 Kila mmoja alikuwa na nyuso nne; uso wa kwanza ulikuwa uso wa kerubi, na uso wa pili ulikuwa uso wa mwanadamu, na uso wa tatu ulikuwa uso wa simba, na uso wa nne ulikuwa uso wa tai.

Ezekieli 17 : 3
3 useme, Bwana MUNGU asema hivi; Tai mkubwa, mwenye mabawa makubwa na manyoya marefu katika mabawa, mwenye kujaa manyoya, yaliyo ya rangi mbalimbali, alifika Lebanoni, akakitwaa kilele cha mwerezi;

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *