Biblia inasema nini kuhusu Shoka – Mistari yote ya Biblia kuhusu Shoka

Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia Shoka

Kumbukumbu la Torati 19 : 5
5 kama aingiapo mtu na mwenziwe mwituni kwenda kukata kuni, akapeleka mkono wake na shoka ili kukata mti, likatoka shoka katika mpini, likampiga yule mwenziwe hata akafa; basi na akimbilie katika miji hii mmojawapo awe hai;

1 Samweli 13 : 21
21 Na walilipa theluthi mbili za shekeli kunoa jembe na miundu, na theluthi moja ya shekeli kunoa mashoka na kuchonga michokoo.

2 Samweli 12 : 31
31 Naye akawatoa watu waliokuwamo, akawaweka kwenye kazi ya[10] misumeno, na sululu za chuma, na mashoka ya chuma, akawafanyiza kazi tanurini mwa matofali; ndivyo alivyoifanya miji yote ya wana wa Amoni. Kisha Daudi akarudi na watu wote Yerusalemu.

Zaburi 74 : 6
6 Na sasa nakishi yake yote pia Wanaivunjavunja kwa mashoka na nyundo.

2 Wafalme 6 : 6
6 ⑰ Mtu wa Mungu akasema, Kilianguka wapi? Akamwonesha mahali. Akakata kijiti, akakitupa pale pale, chuma kikaelea.

Ezekieli 26 : 9
9 Naye ataweka vyombo vyake vya kubomolea mbele za kuta zako, na kwa mashoka yake ataiangusha chini minara yako.

Yeremia 46 : 22
22 Sauti yake ni kama nyoka, wajapo kwa nguvu, Watamjia na mashoka, kama wachanja kuni.

Yeremia 51 : 20
20 ⑮ Wewe ni rungu langu na silaha zangu za vita; kwa wewe nitawavunjavunja mataifa; na kwa wewe nitaharibu falme;

Mathayo 3 : 10
10 ⑩ Na shoka limekwisha kuwekwa penye mashina ya miti; basi kila mti usiozaa matunda mazuri hukatwa na kutupwa motoni.

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *