Hizi ndizo Aya za Biblia zinazozungumzia Sheria
Zaburi 19 : 9
9 Kicho cha BWANA ni kitakatifu, Kinadumu milele. Hukumu za BWANA ni kweli, Zina haki kabisa.
Zaburi 119 : 8
8 Nitazitii amri zako, Usiniache kabisa.
Mithali 28 : 5
5 Watu waovu hawaelewi na haki; Bali wamtafutao BWANA huelewa na zote.
Mathayo 22 : 21
21 Wakamwambia, Ni ya Kaisari. Akawaambia, Basi, mpeni Kaisari yaliyo ya Kaisari, na Mungu yaliyo ya Mungu.
Luka 20 : 25
25 Akawaambia, Basi, vya Kaisari mpeni Kaisari, na vya Mungu mpeni Mungu.
Luka 16 : 17
17 Lakini ni rahisi zaidi mbingu na nchi vitoweke, kuliko itanguke nukta moja ya torati.
Warumi 2 : 15
15 ⑥ Hao waionesha kazi ya torati iliyoandikwa mioyoni mwao, dhamiri yao ikiwashuhudia, na mawazo yao, yenyewe kwa yenyewe, yakiwashitaki au kuwatetea;
Warumi 7 : 7
7 ④ Tusemeje, basi? Torati ni dhambi? La hasha! Lakini singalitambua dhambi ila kwa sheria; kwa kuwa singalijua kutamani, kama torati isingalisema, Usitamani.
Warumi 7 : 12
12 ⑧ Basi torati ni takatifu, na ile amri ni takatifu, na ya haki, na njema.
Warumi 7 : 14
14 ⑪ Kwa maana twajua ya kuwa torati asili yake ni ya rohoni; bali mimi ni mtu wa mwilini, nimeuzwa chini ya dhambi.
Warumi 13 : 10
10 ⑤ Pendo halimfanyii jirani neno baya; basi pendo ndilo utimilifu wa sheria.
1 Timotheo 1 : 5
5 Lakini lengo la agizo hili ni kuleta upendo utokao katika moyo safi na dhamiri njema, na imani isiyo na unafiki.
1 Timotheo 1 : 10
10 na wazinifu, na wafiraji, na waibao watu, na waongo, nao waapao kwa uongo; na linginelo lolote lisilopatana na mafundisho ya kweli;
Yakobo 1 : 25
25 Lakini aliyeitazama sheria kamilifu iliyo ya uhuru, na kukaa humo, asiwe msikiaji msahaulifu, bali mtendaji wa kazi, huyo atakuwa heri katika kutenda kwake.
1 Yohana 3 : 4
4 ⑦ Kila atendaye dhambi, afanya uasi; kwa kuwa dhambi ni uasi.
Kumbukumbu la Torati 1 : 1
1 Haya ndiyo maneno Musa aliyowaambia Israeli wote ng’ambo ya Yordani nyikani, katika Araba lililoelekea Sufu, kati ya Parani, na Tofeli, na Labani, na Hazerothi, na Dizahabu.
Kumbukumbu la Torati 4 : 13
13 ⑭ Akawahubiria agano lake, alilowaamuru kulitenda, yaani, zile amri kumi; akaziandika katika vibao viwili vya mawe.
Kumbukumbu la Torati 33 : 2
2 ⑬ Akasema, BWANA alitoka Sinai, Akawajia kutoka Seiri; Aliangaza katika kilima cha Parani, Akaja Meribath-kadeshi. Upande wa mkono wake wa kulia Palikuwa na sheria ya motomoto kwao.
Habakuki 3 : 3
3 Mungu alikuja kutoka Temani, Yeye aliye mtakatifu kutoka mlima Parani. Utukufu wake ukazifunika mbingu, Nayo dunia ikajaa sifa yake.
Leave a Reply